Skip to main content

Mwenyekiti aliyefungwa miaka 15 aachiwa

KIJIJI cha Msitu wa Mbogo wilayani Arumeru mkoani Arusha, jana kililipuka kwa furaha baada ya viongozi wanne wa kijiji hicho, akiwemo mwenyekiti, kuachiwa huru kwa dhamana na Mahakama.

Waliachiwa baada ya siku 20 za vilio, simanzi na majonzi za wakazi wa kijiji hicho kuhusu suala la viongozi hao. Viongozi hao, Mwenyekiti wa Kijiji, Ernest Mkilanyi na wajumbe wake wanne, walihukumiwa jumla ya miaka 75 jela hivi karibuni kwa unyang’anyi wa Sh 780,000.

Kila mtu alihukumiwa miaka 15 jela. Kuachiwa kwa dhamana kwa viongozi hao kunatokana na juhudi za Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Husna Mwilima na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama katika kushughulikia rufaa dhidi ya hukumu hiyo, iliyotolewa na Hakimu John Mwita wa Mahakama ya Mwanzoya Mbuguni/Maji ya Chai .

Mwilima aliwaahidi wananchi hao, walipoandamana hadi ofisini kwake Aprili 10 mwaka huu kupinga hukumu hiyo na kumuomba kuwapatia tena viongozi wao kwa kuwarejesha uraiani.

Akizungumza jana katika mkutano wa hadhara na mapokezi ya mwenyekiti huyo na viongozi wenzake wa Serikali ya Kijiji, Mkuu huyo wa Wilaya alisema yeye na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama waliamua kuingilia kati hukumu hiyo kwa kukata rufaa,

kutokana na kutoridhishwa na mwenendo mzima wa kesi. Alisema anatambua Mahakama ni mhimili kati ya mihimili mitatu ya nchi unaojitegemea, lakini aliutaka kutenda haki katika kazi zake na wao kama mhimili mwingine ambao ni serikali, hautasita kuingilia kati jambo ambalo wataliona halijakwenda sawa.

Mkuu huyo aliongeza kuwa, kutokana na mazingira ya kesi hiyo aliwaagiza Mwanasheria wa Halmashauri, Katibu Tawala wa Wilaya na Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa wilayani humo, kufuatilia jambo hilo na kuweka mazingira ya kukata rufaa.

Alisema kazi hiyo ilifanyika vyema na ndipo wawili kati ya watuhumiwa hao watano, Julius Nyangusi na Edwin Deo walipofutiwa hukumu na kuachiwa huru, kwa kuwa hawakuhudhuria mahakamani hata siku moja tangu kesi hiyo ilipoanza kusikilizwa.

Mwilima alisema kutokana na rufaa hiyo kukubaliwa, ndipo walipowasilisha maombi mengine ya kuachiwa kwa dhamana washitakiwa wawili wakati rufaa yao ikisikilizwa, ambao ni mwenyekiti huyo na Juma Maulid, wakati Simon Simon akiendelea kubaki gerezani, kutokana na kukabiliwa na kesi nyingine ya mauaji.

Hata hivyo kutokana na mazingira ya kesi yenyewe, wataendelea kuishughulikia kwa kuwa imegubikwa na mazingira yasiyoeleweka dhidi ya watuhumiwa na harakati walizokuwa wakizifanya dhidi ya mwekezaji wa shamba la Tanzania Plantation, Pradep Zodia na masuala ya uchaguzi wa Oktoba mwaka huu.

Mkuu huyo wa Wilaya aliwaeleza wananchi hao kuwa tayari timu kutoka Wizara ya Ardhi imeshawasili wilayani humo, kuanza kufanyia kazi mgogoro huo na aliwataka wawe watulivu wakati kazi hiyo ikiendelea.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya alifananisha tukio hilo la kuhukumiwa miaka 15 jela kuwa ni sawa na Yona katika kitabu cha Biblia, ambaye alimezwa na samaki na kisha kutemwa tena na kwamba kamwe hatarudi nyuma kutokana na vitisho hivyo.

Aidha, aliwataka wananchi wake kuwa watulivu katika kipindi cha kusikilizwa kwa rufaa yake kwa kuachana na matendo, ambayo yanaweza kuharibu mwenendo wa kesi hiyo na kuonekana yamefanyika kwa yeye kuwatuma au kwa sababu yupo nje kwa dhamana

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.