Skip to main content

Tanroads yaagizwa kukabidhi barabara kwa DART

Magufuli ameagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kukabidhi maeneo ya barabara yaliyokamilika ya mradi wa barabara wa mabasi yaendayo kasi kwa Wakala wa Usafiri Haraka wa Mabasi(DART) ili yaanze kutumiwa na wananchi.

Aidha ameiagiza kampuni inayojenga mradi huo ya Strabag kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha mradi huo haraka ambapo hadi sasa umekamilika kwa asilimia 90.

Dk Magufuli aliyasema hayo jana Dar es Salaam baada ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka (BRT) kutoka Morocco - Magomeni - Fire hadi Kariakoo na kuweka jiwe la msingi katika Barabara ya Uhuru.

Pia aliiagiza DART kuhakikisha mchakato wa kupata magari ili wanapokabidhiwa barabara hizo magari yaanze kufanya safari badala ya kupoteza muda mwingine wa kusubiri mabasi.

Alisema Dar es Salaam ni Mkoa ambao unatekeleza miradi mingi ya miundombinu ambapo kwa miradi inayotekelezwa kwa sasa na inayotarajiwa kujengwa inakaribia thamani ya Sh trilioni nne.

Alisema katika mradi wa barabara za juu zabuni zitafunguliwa mwaka huu na ambapo pia fedha za ujenzi wa daraja la Selander litakalopita baharini zimeshapatikana na ujenzi wake utaanza mwaka huu.

Mapema Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Patrick Mfugale alisema mradi huo umepangwa kutekelezwa katika awamu sita, ambapo katika awamu ya kwanza umekamilika kwa asilimia 90 na utagharimu Sh bilioni 369 ambazo zinatolewa na Benki ya Dunia kama mkopo wa riba nafuu.

Disqus seems to be taking longer than usual. Reload?

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...