Skip to main content

Albino mwingine akatwa mkono

MWANAMKE mwenye ulemavu wa ngozi (albino), Remi Luchoma (30), mkazi wa kijiji cha Mwamachoma kata ya Mamba wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi, amekatwa mkono wake wa kulia na watu wasiojulikana, kisha wakatokomea na kiganja cha mkono huo kusikojulikana.

Kwa sasa, mtu huyo amelazwa katika Hospitali ya wilaya ya Mpanda kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda, Dk Joseph Mkemwa alithibitisha kumpokea mama huyo na kwamba anapatiwa matibabu na hali yake inaendelea vizuri.

Alieleza kuwa tukio la kukatwa mkono wa albino huyo, lilitokea hapo jana majira ya saa 6 usiku nyumbani kwa wazazi wake katika kijiji hicho.

Alisema baada ya kukatwa kiganja chake cha mkono wa kulia, albino huyo alipelekwa katika Kituo cha Afya cha Mamba, ambapo alipewa rufaa na kukimbizwa katika Hospitali ya wilaya ya Mpanda kwa ajili ya matibabu zaidi.

Alipokewa katika hospitali hiyo ya wilaya saa 10 alfajiri na amelazwa wadi namba mbili .Hali yake inaendelea vizuri.

Kwa upande wake, Masuma Luchuma ambaye ni kaka wa albino huyo, alisema tukio hilo la dada yake kukatwa kiganja cha mkono ni la kinyama na limemsikitisha. Alisema tukio hilo lilitokea kwenye chumba alichokuwa akiishi albino huyo, mwenye watoto wanne.

Kaka huyo alisema siku ya tukio majira ya saa 6 usiku, alisikia watu wakivunja mlango wa chumba alichokuwa amelala Remi na baada ya muda mfupi, alisikia dada yake huyo akipiga mayowe ya kuomba msaada.

Alidai alijaribu kutoka nje ili kumwokoa dada yake huyo, lakini alishindwa kutoka nje kwa kuwa watu hao walifunga mlango wake kwa nje. Alisema hali ya kufungiwa ndani, ilimfanya apige kengele ya jembe, kama ishara ya kuomba msada kwa majirani .

Hali hiyo iliwafanya watu hao, wakimbie na kutokomea kusikojulikana.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahri Kidavashari alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba wanaendelea na msako mkali kuwasaka waliohusika na tukio hilo

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...