Skip to main content

Bilioni 8 Kutumika Kupanga Upya Jiji la Mwanza

SERIKALI inakusudia kutumia Sh bilioni nane katika mpango wake wa kulipanga upya Jiji la Mwanza kwa kuainisha sehemu za makazi, viwanda, biashara na huduma za kijamii.

Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa jana na Mkurugenzi Msaidizi wa Mpango Mkakati wa Kuyapanga Majiji kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mahenge Amulike, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau na viongozi wa Serikali wa sekta zote wa kupokea maoni na mapendekezo ya kuainisha maeneo hayo.

Pia aliwataka wakazi wa Mwanza na Arusha kutambua hakuna haja ya kumiliki  eneo kubwa la ardhi kwa ajili ya kujenga nyumba nyingi badala yake wanapaswa kumiliki eneo dogo ili kujenga ghorofa.

Alisema Serikali imeamua kuainisha maeneo ya majiji hayo kwa sababu ya ardhi kutoongezeka huku watu wakiongezeka kwa kasi hivyo ni lazima maeneo yakapangwa katika utaratibu unaotakiwa ikiwa ni kuepusha majanga yanatokana na watu kuishi katika maeneo hatarishi bila wao kujua.

Alisema tatizo kubwa lilipo kwa  Watanzania ni kutaka kumiliki eneo kubwa la kujenga nyumba kitendo kinachosabisha  watu wengine kukosa ardhi na kukosekana sehemu ya kuweka huduma za kijamii.

“Watu wanaongezeka kwa kasi lakini ardhi ipo pale pale tena mahitaji yanaongezeka, sasa bila kuyapanga majiji hayo kutakuwa na hatari mbeleni, lazima ardhi igawanywe kwa utaratibu unaokubalika, ni vema umiliki viwanja viwili kwa kujenga ghorofa 10 hadi 20 kuliko kumiliki ardhi kubwa na kujenga nyumba nyingi.

“Wapo watu wanaoishi milimani na mabondeni hao wapo hatarini, chukulia asilimia 70 ya wakazi wa Mwanza wanaishi milimani palipo na mawe, sasa jiwe la asili halitakiwi kuguswa au kuchimbwa lakini watu wamejenga nyumba juu ya mawe, ndiyo maana tunasikia yanaporomoka na hao maisha yao yapo hatarini,” alisema Amulike.

Alisema Serikali ya Tanzania ilisaini mkataba Januari 15 mwaka huu na watalaamu wa mipango miji kutoka Singapore ili kuyapanga majiji ya Arusha na Mwanza na ndani ya miezi 19 watashughulikia kuainisha na kupanga maeneo hayo.

Alisema baada ya kazi ya kuainisha kukamilika utaanza kutekelezwa na utakuwa na mkataba mwingine.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...