Skip to main content

Chadema Wazuiwa Kuhudhuria Mikutano ya CCM

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Momba, Mkoa wa Mbeya, kimewapiga marufuku wanachama wake wasihudhurie mikutano ya hadhara ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wito huo umetolewa juzi na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA), Wilaya ya Momba, Ayubu Sikagonamo, alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Kata ya Sogea.

Sikagonamo alitoa agizo hilo baada ya wanachama wa chama chake kudaiwa kupigwa na wanachama wa CCM hivi karibuni.

“Ili kuondokana na vurugu zinazoweza kuepukika, wanachama wetu mnatakiwa kutohudhuria mikutano inayoitishwa na CCM, hata kama wamewafuata katika maeneo mnayofanyia kazi zenu.

“Yeyote atakayekwenda katika mikutano ya CCM na kupigwa na wanachama wa CCM, hatutashughulika naye kwa sababu atakuwa amejitakia mwenyewe.

“Wananchi wote kwa muda huu tunaoelekea kwenye uchaguzi mkuu, kila mmoja awe tayari kukiunga mkono chama chake na siyo kuwashabikia wengine,” alisema Sikagonamo.

Pia aliwataka wafuasi wa chama hicho wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, ili waweze kuwa na sifa za kuwachagua wagombea wa Chadema na wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Naye Katibu wa BAVICHA, Wilaya ya Momba, Hoseah Kibwana, alilitaka Jeshi la Polisi kutokitetea chama chochote cha siasa kwa kuwa hilo siyo jukumu lake.

Aliwataka wagombea wa CCM wanaotaka kugombea ubunge katika Jimbo la Mbozi Magharibi linaloongozwa na Chadema, wasiendelee kupoteza muda kwa kuwa hawatashinda.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...