OFISI ya Madini wilayani Chunya mkoa wa Mbeya imekusanya mrabaha wa Sh milioni 719.7 kutokana na dhahabu iliyozalishwa wilayani humo katika kipindi cha Julai 2014 hadi Aprili 2015.
Ofisa Madini Mkazi katika wilaya ya Chunya, Ronald Mremi alimweleza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage kuwa katika kipindi hicho, ofisi hiyo pia imefanikiwa kukusanya kiasi ch Sh milioni 187.6 ikiwa ni makusanyo yanayotokana na ada mbalimbali.
Mwijage alikutana na baadhi ya watendaji wa halmashauri hiyo, akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya umeme ya awamu ya pili inayotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kushirikiana na Wakala wa Nishati Vijijini ( REA) katika Kanda ya Kusini.
Kuhusu utengaji wa maeneo kwa wachimbaji wadogo katika wilaya hiyo, Mremi alisema Wizara ya Nishati na Madini imetoa maeneo mawili, mojawapo ni eneo la Itumbi B lenye ukubwa wa kilometa za mraba 12.78 ambapo lilifanyiwa michoro ya kukata viwanja na kupata viwanja zaidi ya 300
Comments
Post a Comment