Skip to main content

Jaji anusurika vurugu za bodaboda

Written by Peti Siyame, Sumbawanga
Hits: 603

JAJI Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, Kasukulo Sambo juzi alinusurika katika mapambano yaliyoibuka eneo la Soko Kuu mjini hapa mkoani kati ya askari polisi na madereva wa pikipiki za magurudumu matatu maarufu kama Bajaj, baada ya madereva hao kugoma na kufunga barabara kwa kulala kifudifudi.

Kitendo hicho kilisababisha kusimama kwa huduma ya usafiri katika barabara kuu inayounganisha mji ya Sumbawanga na Tunduma kwa saa kadhaa na kusababisha askari polisi kufyatua risasi hewani na kurusha mabovu ya machozi ili kuwatawanya.

Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) walifika eneo hilo la tukio wakiwa na silaha nzito wakitumia usafiri wa gari lao lenye namba PT 1854 tayari kukabiliana na mgomo huo .

Licha ya madereva hao kulala kifudifudi barabarani, pia waliweka mbao zilizopigiliwa misumari kuzuia gari lolote lisipitie eneo hilo la tukio na kuchoma matari ya magari.

Miongoni mwa watumiaji wa barabara waliokumbwa na adha hiyo ni Jaji Sambo ambaye gari lake lilizuiwa na kunusurika kushambuliwa na madereva hao waliokuwa wamejawa na ghadhabu.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Jaji Sambo alithibitisha kutokewa na mkasa huo na kwamba maofisa askari wa usalama barabarani waliingilia kati na hatimaye akaruhusiwa kupita eneo hilo na gari lake .

“Nilipofika eneo hilo nilikuwa madereva wa bajaji wakiwa wamegoma wakitaka kuonana na Mkuu wa Mkoa kwa kufunga barabara kuu …..walinizuia nisipite hadi askari polisi wa usalama barabara alipoingilia kati pia mlinzi wangu alilazimika kushuka gari akiwa tayari na bastola kwa kujihami…. “Hatimaye niliweza kupita hapo salama saliminik lakini mkasa huo umesababisha adha kubwa kwa watumiaji wengine wa barabara,“ alieleza Jaji Sambo.

Shughuli za kawaida katika soko kuu la mjini Sumbawanga zilisimama kwa muda wa saa moja baada ya jeshi la polisi mjini hapo kuvutana juu ya mgomo wa ghafla ulioitishwa na madereva wa pikipiki za magurudumu matatu maarufu kwa jina la bajaji.

Kaimu Kamanda Polisi mkoa wa Rukwa, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Leons Rwegasira amethibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kueleza kuwa bado jeshi hilo linatumia busara kulishughulikia tatizo hilo kabla ya kuanza kamata kamata.

Aliongeza kuwa hakuna majeruhi aliyeripotiwa wala uharibifu wowote uliotokana na vurugu hizo ambapo aliwasihi vijana kuacha kujichulia sheria mkononi na kuanza kurusha mawe kwenye gari la polisi.

Vurugu hizo zilizodumu kwa zaidi ya saa moja zimetokea leo saa sita mchana ambapo madereva hao wa bajaj wanaotoa huduma za usafiri katika Manispaa ya Sumbawanga na vitongoji vyake vilisababisha taharuki kubwa kwa wakazi wa mjini humo.

Mwenyekiti wa madereva hao, Fred Jackson alisema wameamua kugoma kutokana na utaratibu wanaoutumia askari wa usalama barabarani mjini Sumbawanga ambapo kila siku wamekuwa wakipanga kiwango cha makusanyo ya fedha kutoka kwao na hivyo kulazimisha makosa yasiyokuwapo.

Alisema wameshajipanga kugoma mpaka uongozi wa serikali utakapoyashughulikia malalamiko yao ikiwa ni pamoja na kuwabaini askari wa usalama barabarani wanaofanya ukamataji kwa lengo la kujipatia kipato na siyo kusimamia sheria.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...