Skip to main content

JK akerwa vijana nchini kutumika na wazee

TABIA ya vijana wa sasa ya kuchukua fedha kutoka kwa wazee na kuwagawia vijana wenzao ili kurahisisha mambo kwa wazee hao, imeonesha kumkera Rais Jakaya Kikwete.

Akizungumza na vijana mjini hapa alisema vijana wa zamani walikuwa tofauti na wa sasa, wakati vijana wakihakikisha mambo yanakwenda vyema na hawatumiki vibaya, wa sasa ndio wanachukua fedha na kuwagawia wenzao.

Alisema tabia ya baadhi ya viongozi wa vijana kutumika kugawa fedha za wazee inaua demokrasia na maadili na kuingiza utamaduni wa hovyo katika siasa.

“Kama ukiwa na viongozi wa vijana unapojihusisha na kugawa fedha, vijana hamuwezi kugeuka makuwadi, hamuwezi kugeuka kuwa mawakala wa kuhonga vijana wenzenu mtakuwa mmetoka kabisa kwenye mstari,” alisema Rais Kikwete.

Alikuwa akifungua mkutano mkuu wa kwanza wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu jana huku akitamba kuwa CCM itaendelea kuongoza na wataisoma namba.

Aliwaasa vijana kuwa hatima ya CCM iko mikononi mwao na hivyo ni vyema wakajiepusha na matendo ya rushwa na ukiukaji wa maadili.

“Hatma ya CCM iko mikononi mwa vijana, Umoja wa Vijana una kazi ya kuandaa vijana, nina masikitiko kwa haya yanayotokea,” alisema.

Alisema shirikisho ni kiungo muhimu kati ya CCM na wanafunzi kwani wanachagua viongozi wa kutengeneza daraja kati ya wanafunzi na chama.

Alisema Umoja wa Vijana una kazi ya kuandaa vijana, kupata wanachama wapya na kuimarisha umoja huo ili uwe na manufaa hapo baadaye

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.