Skip to main content

Jonas Mkude aipa somo Simba

KIUNGO wa Simba, Jonas Mkude ameutaka uongozi wa timu yake kuhakikisha wanafanya usajili makini ili msimu ujao waweze kufanya vizuri na kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Simba imemaliza nafasi ya tatu kwenye ligi ya msimu huu uliomalizika Jumamosi iliyopita na kufanya timu hiyo kumaliza nafasi nje ya mbili bora msimu wa tatu mfululizo na kukosa nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa.

Akizungumza na gazeti hili jana Mkude alisema usajili makini ndiyo utakaobadili mwenendo mbaya wa timu hiyo na kurudisha furaha kwa wachezaji, viongozi na mashabiki wa timu yao ambao kwa muda mrefu imepotea.

“Simba ni timu kubwa, inaumiza kuona tunashindwa kumaliza japo nafasi ya pili naushauri uongozi kuwa makini katika usajili wa msimu ujao ili tubadili mwenendo wetu na kuwa bora kama ilivyokuwa siku za nyuma,” alisema Mkude.

Alisema sehemu kubwa ambayo angependa ifanyiwe marekebisho ni safu ya ulinzi na ushambuliaji ambazo zimeonesha upungufu mkubwa kwenye msimu uliomalizika kwa timu yao kushindwa kutimiza lengo walilojiwekea.

“Pamoja na kuanza vibaya, lakini baadaye tulibadilika na kuweka malengo ya kumaliza angalau nafasi ya pili, lakini pia haikutimia mapungufu yetu makubwa yalikuwa kwenye ulinzi na hata safu ya ushambuliaji ambayo imekosa mshambuliaji wa kuaminika,” alisema Mkude.

Safu ya ulinzi ya Simba msimu uliopita imeruhusu mabao 18 huku ile ya ushambuliaji ikufunga mabao 36 na mshambuliaji wake Emmanuel Okwi, akifunga mabao 10 wakati Ibrahim Ajibu akifunga mabao saba pekee.

Mkude alisema matumaini yake ni kuwa huu ndiyo msimu wa mwisho kupata matokeo mabaya na kumaliza nje ya mbili bora kwenye Ligi ya Bara kutokana na maandalizi pamoja na usajili wanaotarajia kuufanya

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...