Skip to main content

Kamati ya Bunge yaikataa bajeti Maliasili na Utalii

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Maliasili na Utalii jana ilikataa kujadili bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii huku ikiwataka Waziri na watendaji wake kuondoka ukumbi wa mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dar es Salaam ambako walikuwa wakutane kwa majadiliano.

Sababu kubwa imetajwa ni wizara hiyo kushindwa kutekeleza maagizo yaliyotolewa na kamati hiyo, ikiwemo kukaidi amri ya Mahakama Kuu ya kutaka kuanza mara moja utekelezaji wa tozo mpya kwenye Hifadhi za Taifa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu, ya Maliasili na Utalii, James Lembeli alitoa uamuzi huo jana jijini Dar es Salaam wakati kamati hiyo ilipokutana na wizara hiyo chini ya Waziri wake Lazaro Nyalandu ambaye alikiri kuwapo kwa tatizo katika ripoti huku akiahidi kufanyia kazi.

“Hatuwezi kupitia bajeti hii, kwa sababu maagizo tuliyotoa awali hayajatekelezwa, sasa tuna uhakika gani kama tukipitia hii bajeti yao ya mwaka 2015/16, watakwenda kutekeleza tutakachoagiza?” Alihoji Lembeli.

Alisema kimsingi, wizara hiyo imekwenda kinyume na makubaliano yao na kwamba ni vyema wizara hiyo ikaenda kujipanga na kufanya marekebisho ya maagizo yaliyotolewa kisha kurejea kujadili bajeti hiyo.

Lembeli aliyataja maagizo yaliyotolewa na kamati hiyo kuwa ni pamoja na utaratibu wa kiingilio kwenye hifadhi, ambapo tozo iliyotakiwa ni kila mtalii anapoingia anachajiwa kiingilio na akitoka na kutaka kuingia tena ni lazima alipe.

Alisema jambo hilo halizingatiwi na kwamba serikali imeingilia na kufuta tozo hiyo ambayo hivi sasa watalii wanaingia na kutoka na kisha kuingia tena bila kulipa jambo linalokosesha hifadhi mapato.

Kuhusu amri ya Mahakama, Kamati ilimtaka atekeleze agizo lililotolewa na Mahakama kuhusu utekelezaji wa kutoa tangazo kwenye gazeti la serikali kuhusu tozo mpya za kodi za utalii ambapo Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilitoa agizo hilo Septemba mwaka jana na kutaka utekelezaji wake uanzi mara moja.

Lembeli alisema tangu kutolewa na agizo hilo imeshapita miezi kadhaa utekelezaji wake haujafanywa na waziri, jambo ambalo linaokosesha mapato ya Sh bilioni 80 kwa mwaka, Mamlaka ya Hifadhi Tanzania (Tanapa).

Akizungumzia agizo jingine, alisema ni mgogoro wa mipaka kwenye Hifadhi ya Taifa ya Saadan ambapo kamati iliagiza kuwa mipaka ya hifadhi hiyo ibaki kama ilivyokuwa tangu awali, lakini kinyume chake, wizara imemega sehemu ya ardhi na kuitafutia hati miliki.

Waziri Nyalandu alikiri kuwepo na matatizo kwenye maagizo ya ripoti hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi hiyo jana na wataalamu wa wizara hiyo ili wahakikishe wanatatua changamoto hizo, na leo wanaweza kutoa ripoti hiyo ili kamati ijadili bajeti yao.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...