Skip to main content

Kocha Simba Sc kutangazwa leo

KITENDAWILI cha kocha atakayeifundisha Simba msimu ujao kinatarajiwa kuteguliwa leo, wakati jina litakapowekwa hadharani.

Simba ilishindwana na kocha wake Mserbia Goran Kopunovic, aliyeiongoza timu hiyo kumaliza ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliomalizika hivi karibuni.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya timu hiyo, Zacharia Hanspoppe alisema jana kuwa, leo wanatarajia kutangaza jina la kocha huyo baada ya kushindwana na yule wa awali.

Ilidaiwa kuwa Kopunovic alikuwa akitaka kiasi kikubwa cha fedha ili kusaini mkataba mpya wa miaka miwili na Simba ilikuwa ikimtaka kocha huyo kwa miezi tisa.

Awali, kocha huyo alikuwa na mkataba wa miezi sita, uliomalizika Jumapili ya wiki iliyopita baada ya ligi kufikia tamati.

Awali, Simba ilisema kuwa kulikuwa na majina ya makocha sita waliojitokeza kujaza nafasi ya kocha huyo Mserbia aliyetaka kiasi cha dola za Marekani 50,000 (ambazo ni sawa na Sh milioni 100) kwa ajili ya kusaini mkataba.

Pia, kocha huyo inadaiwa alihitaji kiasi cha dola 8,000 kwa ajili ya mshahara wake wa mwezi, lakini Simba ikashindwa kukubaliana na masharti hayo ya kocha huyo.

Hatahivyo, Simba haikuwataja makocha hao sita walioomba kibarua cha kuinoa timu hiyo, ambayo haijashiriki mashindano ya kimataifa kwa misimu mitatu mfululizo baada ya kushindwa kumaliza ligi ndani ya mbili bora.

Ilielezwa kuwa makocha hao sita wangepunguzwa hadi kufikia wawili, ambao wangechuana kwa vigezo ili kumrithi kocha huyo aliyemaliza muda wake.

Simba imesema kuwa iko makini katika mchakato huo wa kusaka kocha ili kuiwezesha timu hiyo kufanya vizuri msimu ujao na kuweza kupata moja kati ya nafasi mbili za kwanza zitakazoiwezesha kushiriki mashindano ya kimataifa.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...