Skip to main content

Kocha Simba Sc kutangazwa leo

KITENDAWILI cha kocha atakayeifundisha Simba msimu ujao kinatarajiwa kuteguliwa leo, wakati jina litakapowekwa hadharani.

Simba ilishindwana na kocha wake Mserbia Goran Kopunovic, aliyeiongoza timu hiyo kumaliza ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliomalizika hivi karibuni.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya timu hiyo, Zacharia Hanspoppe alisema jana kuwa, leo wanatarajia kutangaza jina la kocha huyo baada ya kushindwana na yule wa awali.

Ilidaiwa kuwa Kopunovic alikuwa akitaka kiasi kikubwa cha fedha ili kusaini mkataba mpya wa miaka miwili na Simba ilikuwa ikimtaka kocha huyo kwa miezi tisa.

Awali, kocha huyo alikuwa na mkataba wa miezi sita, uliomalizika Jumapili ya wiki iliyopita baada ya ligi kufikia tamati.

Awali, Simba ilisema kuwa kulikuwa na majina ya makocha sita waliojitokeza kujaza nafasi ya kocha huyo Mserbia aliyetaka kiasi cha dola za Marekani 50,000 (ambazo ni sawa na Sh milioni 100) kwa ajili ya kusaini mkataba.

Pia, kocha huyo inadaiwa alihitaji kiasi cha dola 8,000 kwa ajili ya mshahara wake wa mwezi, lakini Simba ikashindwa kukubaliana na masharti hayo ya kocha huyo.

Hatahivyo, Simba haikuwataja makocha hao sita walioomba kibarua cha kuinoa timu hiyo, ambayo haijashiriki mashindano ya kimataifa kwa misimu mitatu mfululizo baada ya kushindwa kumaliza ligi ndani ya mbili bora.

Ilielezwa kuwa makocha hao sita wangepunguzwa hadi kufikia wawili, ambao wangechuana kwa vigezo ili kumrithi kocha huyo aliyemaliza muda wake.

Simba imesema kuwa iko makini katika mchakato huo wa kusaka kocha ili kuiwezesha timu hiyo kufanya vizuri msimu ujao na kuweza kupata moja kati ya nafasi mbili za kwanza zitakazoiwezesha kushiriki mashindano ya kimataifa.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...