Mashabiki ambao ndiyo wapiga kura, bado wanajiuliza kwa nini majina ya wasanii kadhaa ambao walitamba, yamekosekana. Tatizo ni nini?
SHARE THIS STORY
0
inShare
Kuna majina ukikutana nayo katika orodha ya wateule wanaowania Tuzo za Muziki za Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA), unaanza kuyalinganisha na yale maarufu yaliyong’ara mwaka 2014, lakini hayamo katika tuzo za mwaka huu.
Mashabiki ambao ndiyo wapiga kura, bado wanajiuliza kwa nini majina ya wasanii kadhaa ambao walitamba, yamekosekana. Tatizo ni nini?
Katika kipengele cha mwimbaji bora wa kiume wa bendi, majina yaliyoingia ni Jose Mara, Kalala Junior, Khalidi Chokoraa, Chaz Baba na Nyoshi El Sadat. Lakini bado mashabiki wanajiuliza ni kwanini jina la Christian Bella halikuingia wakati ndiye ambaye kwa mwaka mzima alifanya vitu vikubwa na nyimbo zake bado zinatamba.
Minong’ono iliyokuwapo ilidai kuwa Bella hafai kuwapo kwa waimbaji wa kundi kwa kuwa anasimama mwenyewe. Ukweli ni kwamba Bella yupo katika bendi ya Malaika na mara nyingi bendi hii imekuwa ikiitwa Christian Bella and Malaika Band na mwaka jana ilitamba na kibao cha “Nakuhitaji”.
Hata kama nyimbo nyingine alirekodi peke yake bila ya bendi ya Malaika, bado muziki wake ni wa bendi, inashangaza kwamba waandaaji wamelipuuza hilo. Kipengere kingine kilichozua maswali ni Mtunzi Bora wa Mwaka wa Bendi ambacho Bella pia ametemwa, licha ya kutunga nyimbo nyingi zilizokubalika kama “Nani Kama Mama” ambao hakuna ubishi kuwa una sifa zote za kuwa Wimbo Bora wa 2014. Badala yake wameingia akina Jose Mara, Nyoshi El Saadat, Rogart Hegga Katapila, Hussein Jumbe na Richard Mangustino, ambao wengi hawakuwa na kazi zozote mwaka jana.
Katika tuzo ya Mwimbaji Bora wa Kike wa Bendi, hakukuwa na wateule, lakini katika macho ya haraka kuna nyimbo kama “Kariakoo” wa Skylight Band ndani yake kuna mkono wa Aneth Kushaba. Ilishindikana nini kuwamo. Kuna wanamuziki kama Luiza Mbutu, Taji na wengineo ambao walifanya vizuri mwaka 2014.
Kwa upande wa Wimbo Bora wa Taarabu kulikuwa na nyimbo mbili pekee zilizopita ukiwamo wa “Hasid Hana Sababu” wa Hadija Yussuf na “Lady With Confidence” wa Khadija Kopa. Hili ni eneo ambalo lilikuwa na kazi nyingi zilizotamba pengine kazi ingekuwa ni kuzipunguza hadi zibakie tano.
Hii ni kwa mujibu wa jarida la Starehe, lakini wadau walikuwa na mengi ya kuelezea.
Josephat Kambi, mmoja wa mashabiki wa muziki, anauliza: “Katika upande wa tuzo za utunzi bora, sijajua ni vigezo gani vinavyotumika kwa kuwa wapo wasanii tunawajua hawawezi kutunga wimbo mzuri, ila kuna wasanii ambao wanatunga na kuimba. Mfano mzuri ni Barnabas. Kuna kila haja ya wasanii wetu wanapotoa wimbo wataje na mtunzi ili watunzi hawa washirikishwe pia kama kina Ude Ude wametunga nyimbo nyingi za Lady Jaydee, Ali Kiba na wengine.”
Wasanii
Mo Music amejitoa katika kinyang’anyiro hicho tangu wateule watangazwe Aprili.
“Nimeingia katika kipengele cha kuwania Wimbo Bora wa Zouk/Rhumba wa mwaka, ilhali mimi ni msanii chipukizi majibu yake nimewekwa na vigogo kama kina Diamond, Lady Jaydee, Bella na wengineo,” alilalamika.
Comments
Post a Comment