Skip to main content

Ligi Kuu isiendeshwe kimazoea

LIGI Kuu ya Tanzania Bara inakamilika leo huku jambo kubwa ambalo wakuu wanaoendesha ligi hiyo wameshindwa kulipatia jibu sahihi ni kuitangaza ligi hiyo pamoja na mipango mbadala.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi Tanzania bado hawana mbinu mpya za kuweza kuiendesha ligi hiyo kisasa na kilichobaki ni kuiendesha kimazoea tu kama ilivyokuwa hapo awali. Ninasema hivyo kutokana na hali ilivyokuwa inaenda msimu mzima wa ligi hiyo kuanzia ilipoanza Septemba 20, mwaka jana hadi inafikia tamati leo Mei 9, 2015.

Kuna baadhi ya michezo ilikuwa inakosa mashabiki kabisa huku wenyewe wakiwa na kisingizio eti kwa sababu michezo inaoneshwa kwenye runinga basi mashabiki wanashindwa kwenda uwanjani. Huo ni uongo maana tumeshuhudia kwenye nchi nyingi michezo ikirushwa kwenye runinga na mashabiki wanaenda uwanjani.

Niwakumbushe tu kuwa kuna tofauti kubwa ya kuangalia mpira kwenye runinga na kuangalia mpira ukiwa uwanjani kwa sababu ukiwa uwanjani unapata mambo mengi na ukiangalia kwenye runinga kuna mambo mengi unakosa kuyaona. Wale wazoefu na haya mambo wataungana nami kwenye hili.

Hapa tatizo ni mfumo na mbinu mpya kutoka kwa wakuu wa ligi hiyo na kama nilivyosema hapo juu wao wanaongoza ligi hiyo kimazoea, wamekosa mtazamo mpya na wa kisasa. Kuna michezo miwili iliyochezwa katikati ya wiki nilitazama online kwenye runinga ya timu mbili kubwa za Simba na Yanga iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambayo uwanja ulikuwa mweupe kabisa.

Mechi ya kwanza ilikuwa Yanga na Stand United ya Shinyanga na Simba walicheza na Mgambo JKT ya Tanga yaani michezo hii ilikuwa na mashabiki wachache mno ukiongeza na ule mchezowa Mgambo JKT dhidi ya Azam FC uliochezwa jijini Tanga. Ninaweza kusema hii michezo ilitia fora kabisa hasa kutokana na ukubwa wa timu zenyewe.

Hapa jibu ni jepesi tu. Katikati ya wiki utampeleka nani uwanjani akatazame mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara wakati yupo kwenye harakati zake za kusaka mkate wake wa kila siku na hilo ndio jibu sahihi.

Tena ukizingatia muda wenyewe wa mchezo ndio hatari kabisa maana michezo hiyo ilianza mida ya saa kumi jioni ambayo wengi wao wanatoka katikati ya jiji kuelekea makwao na ukiongeza na msongamano wa magari au foleni, ndio kikwazo kabisa cha kukosa mashabiki.

Siku za nyuma hapa hapa nilishasema au kushauri kuwa hebu TFF waache panguapangua ya ratiba waje na ratiba ya maana ya uhakika ili michezo karibu yote ya Ligi Kuu ichezwe mwishoni mwa juma ila wenzangu hawa hawakunisikia hadi leo hii ninavyoandika makala haya, tumeshuhudia mechi zikichezwe katikati ya wiki.

Jambo la pili jamani hivi kinashindikana nini michezo mingine ya Ligi Kuu kuchezwa nyakati za jioni kuanzia muda wa saa 12:30 hadi tatu usiku. Nadhani muda hiyo huwezi kukosa mashabiki hasa kwenye miji ya pwani ya Bahari ya Hindi ambao wao kutoka nyakati za jioni ni tamaduni yao.

Hebu fikiria mechi kama zinahusu timu kubwa za Yanga na Simba eti inakosa mashabiki, si tatizo hili jamani maana timu hizo ndio timu kongwe ambazo zinaungwa mkono na mashabiki wengi wa soka nchini.

Hapa kuna tatizo kwenye Kitengo cha Masomo cha TFF au Bodi ya Ligi Kuu ambao wameshindwa kabisa kuja na mbinu mpya za kuitangaza ligi hiyo kwa mbinu za kisasa na wasipofanya hivyo, wakaendelea kufanya kazi kimazoea, basi hali itaendelea kuwa mbaya zaidi.

Ombi langu kwenu ni kuona ligi hiyo inabadilika na kwenda kisasa kama zilivyo kwenye nchi zingine na niwakumbushe tu kuwa kwenye ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, hapa nyumbani Tanzania ndio nchi pekee yenye mashabiki wengi wa soka wenye wazimu wa ligi ya nyumbani kwa sasa kuliko nchini zingine za jirani.

Hivyo kazi kwenu kuweza kubadili mfumu wa uendeshaji

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...