Skip to main content

Lowassa anguruma kwa niaba ya Bilal

MAKAMU wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal amewataka wakazi wa Jiji la Arusha kuwa na mshikamano wa dhati katika kusimamia suala la amani kwani amani ikipotea hali ya uchumi itayumba.

Kauli hiyo ilitolewa na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kwa niaba ya Makamu wa Rais katika harambee ya ujenzi wa shule ya sekondari na kituo cha kiislamu iliyofanyika katika viwanja vya msikiti mkuu wa Ijumaa Jijini Arusha.

Alisema Jiji la Arusha ni la kitalii lenye muingiliano wa wageni wengi ambao lengo lao ni kwenda kutalii katika mbuga za wanyama hivyo wageni hao hawawezi kukubali kuja nchini hususan katika Jiji la Arusha kama kutakuwa na vurugu na watu kushindwa kufanya shughuli za maendeleo.

Dk Bilal aliwataka wakazi wa Jiji la Arusha kuilinda amani kwa gharama yoyote na kushikamana bila ya kujali dini, kabila wala rangi kwani misingi iliyowekwa ni kwa kila mmoja kumheshimu mwenzake kwa kila namna.

Shehe wa Mkoa wa Arusha, Shabani Juma alisema kuwa lengo la harambee hiyo ni kutaka kukusanya zaidi ya Sh milioni 200 kwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa shule ya sekondari itakayojengwa Patandi Tengeru wilayani Arumeru mkoani Arusha.

Shehe Juma alisema kuwa shule hiyo ambayo itakuwa chini ya Baraza Kuu la Kiislamu nchini (BAKWATA) itakuwa ya wanafunzi wa dini zote na itakuwa ndani ya kituo cha watoto yatima.

Makamu wa Rais na Lowassa na viongozi wengine wa serikali wamechangia harambee hiyo Sh milioni 105 na zaidi ya Sh milioni 140 zimekusanywa katika harambee hiyo zilizotolewa na wafanyabiashara na wanasiasa mbalimbali wa mkoani Arusha na nje ya mkoa.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...