Skip to main content

Madiwani Walia Na Ndoa FEKI Za Walimu......Wadai Upungufu Wa Walimu Vijijini Unasababishwa Na Walimu Wa Kike Kughushi Vyeti Vya Ndoa

BAADHI ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga, wamesema tatizo la upungufu wa walimu kwenye shule za msingi zilizopo vijijini kunachangiwa na walimu hasa wa kike kutaka kufundisha mjini.

Walisema baadhi ya walimu wa kike wamekuwa wakighushi vyeti vya ndoa ili kuonesha wameolewa na kuwafuata waume zao mijini jambo linalozorotesha jitihada za Serikali kumaliza tatizo la walimu kwani baadhi ya shule za vijijini zina walimu hadi wawili.

Madiwani hao waliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo Diwani wa Kata ya Lusanga, Sesiwa Mhando, alidai halmashauri ilitenga sh. milioni 30 kwa ajili ya walimu kupelekwa shule za vijijini; lakini hadi sasa hajui mchakato huo umekwamia wapi.

"Tatizo la walimu kwenye shule za msingi linatokana na walimu kujazana mijini hasa wa kike wakiwa na ndoa   bandia, madiwani tulitenga sh. milioni 30 ili zitumike kupeleka walimu vijijini lakini sijui mchakato huo umeishia wapi," alihoji.

Kwa upande  wake, Kaimu Ofisa Elimu wa Shule za Msingi wilayani humo, Stuart Kuziwa, alisema tatizo la walimu ni la kitaifa likiwemo la kujazana mijini lakini hata shule zilizopo mjini nazo zina upungufu wa walimu.

"Hata shule za mjini nazo zina upungufu wa walimu, tumeomba kupatiwa walimu 230 kwa miaka mitatu mfululizo, hilo linaweza kumaliza shida ya walimu katika shule za msingi," alisema.

Diwani wa Kata ya Bwembera, Kapteni mstaafu Tito Haji, alisema moja ya shule za msingi kwenye kata yake ina walimu wawili.

"Kwenye Kamati ya Fedha,mlidai tatizo la walimu limekwisha sasa iweje leo mnatueleza kuwa tatizo la walimu bado lipo Muheza, Shule ya Msingi Msowelo ina walimu wawili lakini mjini walimu wamejaa," alisema Kapteni Tito.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Amir Kiroboto, alisema madiwani wasilalamikie tatizo la walimu kujaa mijini bali waangalie idadi ya wanafunzi kwani shule nyingi za mjini zina wanafunzi wengi.

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.