Skip to main content

Mahakama:Watoto wa Vigogo BoT Wanaokabiliwa na Tuhuma za Kughushi Vyeti Wana Kesi ya Kujibu

WAFANYAKAZI wanane wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wanaokabiliwa na tuhuma za kughushi vyeti vya kidato cha nne  wamekutwa wana kesi ya kujibu.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi wanane wa upande wa mashtaka na kuona kwamba kuna haja kwa washtakiwa kujitetea.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni Justina Mungai, Christina Ntemi, Siamini Kombakono, Janeth Mahenge, Beata Massawe, Jackline Juma, Philimina Mtagurwa na Amina Mwinchumu.

Uamuzi huo ulitolewa na Hakimu Mkazi, Nyigulila Mwaseba, wakati kesi hiyo inaendeshwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Shadrack Kimaro.

“Mahakama imepitia ushahidi wa mashahidi wanane wa upande wa Jamhuri, imeuona kwamba ushahidi huo una nguvu, hivyo washtakiwa mna kesi ya kujibu, mnatakiwa kujitetea,” alisema Hakimu Mwaseba.

Baada ya kusema hayo mahakama iliahirisha kesi hiyo  hadi Juni 17 na 18 mwaka huu, kwa ajili ya washtakiwa kuanza kujitetea.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, washtakiwa hao wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa hati za uongo kwa mwajiri wao ambaye ni BoT.

Washtakiwa Justina, Beata na Amina wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2001. Christina, Siamini, Janeth na Philimina, wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2002.

Washtakiwa hao wanadaiwa kughushi vyeti hivyo na kutoa hati za uongo BoT kuonyesha vimetolewa na Baraza la Mitihani Tanzania  wakati si kweli.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...