Skip to main content

Malinzi: Kocha hang’oki

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema kuwa hana mpango wa kumfukuza Kocha Mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars, Mart Nooij.

Kwa sasa wadau mbalimbali wa soka wamependekeza kufukuzwa kwa kocha huyo hasa kutokana na kufanya vibaya kwa timu hiyo katika michuano ya Cosafa inayoendelea nchini Afrika Kusini.

Timu hiyo inashiriki michuano hiyo kama mgeni mwalikwa ikiwa pamoja na Ghana, ilifungwa na Madagascar mabao 2-0 katika mchezo wake wa pili wa Kundi B uliofanyika kwenye Uwanja wa Royal Bafokeng mjini Rustenburg.

Awali, Jumatatu wiki hii ilifungwa bao 1-0 na Swaziland katika mechi ya kwanza, hali ambayo inamaanisha kuwa timu hiyo haikupata hata bao moja, kitu ambacho kimewakera mashabiki wengi wa soka.

Lakini wakati Nooij akicheza mechi yake ya 15 juzi na kufungwa sita, kutoka sare sita na kushinda mechi tatu tu tangu Aprili mwaka jana alipoanza kazi, Malinzi anasema licha ya matokeo hayo, haoni sababu ya kumfukuza Mholanzi huyo. Katika mahojiano na gazeti hili jana, Malinzi alisema kwa upande wake anaona kuwa bado kocha huyo anatakiwa kupewa nafasi kwa kuwa bado sio kosa lake moja kwa moja.

Malinzi alisema akiwa Rais anatambua kuwa Watanzania wengi wamekatishwa tamaa na matokeo hayo, lakini kwa upande wake anaiona kuwa bado hiyo ni timu nzuri huku kocha wake akitakiwa kuendelea kupewa muda zaidi.

Alisema kuwa kama kukiwa na utaratibu wa kufukuza makocha hivyo itasababisha kuiharibu timu kwa kuwa sio suala la kubadili kocha ila ni kuangalia mengi zaidi.

Rais huyo aliyemfukuza Kim Poulsen na kumwajiri Nooij miezi michache baada ya kushinda urais wa TFF, alisema timu zilizoifunga Taifa Stars katika Cosafa, sio timu za kawaida ila zimejiandaa na kushiriki michuano hiyo na pia zilikuwa na michuano mingine mikubwa ambayo imetoka kushiriki.

“Mimi ninaona kuwa sio vyema kusema kuwa eti hata Madagascar imetufunga au hata Swaziland imetufunga, hiyo sio vyema kabisa kwa kuwa Swaziland imeshiriki Kombe la Mataifa ya Afrika na imefanya vyema tu, na Madagascar ina makocha zaidi ya 1,000 wanatambuliwa na Fifa sasa sisi hapa hata 100 tu hawajafika,” alieleza Malinzi.

Aliongeza kuwa “kwa kuwa na makocha wengi ina maana kuwa hata timu za kawaida za mitaani zinafundishwa na watu wenye uwezo sasa hapo nataka kumaanisha kuwa sisi tungekuwa na mafanikio hayo leo tungekuwa mbali.”

Malinzi alifikia hatua ya kusema kuwa inatakiwa kuangaliwa zaidi wachezaji labda siku hiyo hawakula chakula au walikuwa hawajapewa posho au pengine viatu vilikuwa vimechakaa na ndio maana wakafungwa.

Aliongeza kuwa Kamati yaUtendaji inakutana keshokutwa kujadili masuala mbalimbali yahusuyo timu hiyo na kuongeza kuwa hakuna sababu ya kulaumiana kwa sasa ila wasubiri Kamati ikikutana ndio majibu yatafahamika.

Alisema Watanzania wanatakiwa kumuunga mkono kocha huyo kwa kuwa uwezo anao na amefundisha timu nyingi ambazo zimekuwa zikifanya vyema hadi sasa.

“Ninafahamu rekodi yake huyu sio kocha wa mchezo kwa kuwa anaweza mengi na sikukurupuka kumtafuta ila nilikuwa najua historia yake kuanzia ameshinda michezo mingapi na sare ngapi na kwetu hapa tuendelee kumpa muda,” alisema Malinzi akimzungumzia kocha huyo mwenye mkataba wa miaka miwili.

Akizungumza baada ya mechi ya juzi, Nooij aliyeiwezesha Msumbiji kucheza fainali za Afcon mwaka 2012, alisema amesikitishwa na matokeo hayo, kwamba hakutegemea kupoteza mchezo dhidi ya Madagascar.

“Timu yangu haikucheza vizuri, haikuweza kutengeneza nafasi nyingi za kufunga huku wapinzani wetu wakitumia nafasi mbili walizozipata kupata mabao mawili katika mchezo huo,” alisema Nooij.

Stars inatarajiwa kurejea nyumbani leo usiku baada ya mchezo wake wa mwisho dhidi ya Lesotho utakochezwa jioni

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...