Afisa Mtendaji Mkuu wa Chuo Cha Utalii Tanzania, Rosada Msoma akizungumza na wanafunzi na wakufunzi wa chuo cha Utalii(hawapo pichani) katika maonyesho ya utalii yaliyofanyika katika chuo hicho kampasi ya Bustani leo jijini Dar es Salaam.
Kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Fedha wa chuo cha utalii Tanzania Neema Kusiga, (watano katikati),Afisa Mtendaji Mkuu wa Chuo Cha Utalii Tanzania, Rosada Msoma akiwa na wakufunzi wa Chuo cha Utalii Tanzania kutoka kampasi tatu za chuo hicho iliyofanyika katika Chuo cha Utalii kampasi ya Bustani jijini Dar es Salaam leo.
Mpishi Issa Haji akitoa maelekezo kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Chuo Cha Utalii Tanzania, Rosada Msoma katika jiko la wanafunzi wanaojifunza kupika vyakula mbalimbali katika Chuo cha Utalii Tanzania Kampasi ya Bustani jijini Dar es Salaam.
Mpishi Issa Haji akitoa maelekezo Kwa wanafunzi wa Chuo cha Utalii cha Wanyamapori kampasi ya Temeke katika maonyesho ya chuo hicho yaliyofanyika katika kampasi ya Bustani leo jijini Dar es Salaam
Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania
Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati Mapinduzi hayo yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada ya tangazo la kupindulikwa kwake, Rais huyo alipanda ndege kurejea nchini kwake licha ya tangazo la kufungwa kwa mipaka yote na viwanja vya...
Comments
Post a Comment