Skip to main content

Matatani kwa bahasha hewa Mei 1

CHAMA cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU), wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa, kimeendelea kuitikisa halmashauri ya wilaya hiyo kikimtuhumu mkurugenzi wake kutoa zawadi ya bahasha tupu kwa watumishi wake 16 bora wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani, Mei Mosi.

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya chama hicho kuibua kile walichoita kashfa ya matumizi mabaya ya fedha za halmashauri hiyo yaliyofanywa na maofisa waliohusika na uandaaji na uwasilishaji wa mpango wa bajeti ya mwaka 2015/2016 jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya Talgwu ambayo pia imethibitishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Ubald Wampembe, jeshi la Polisi limeanza kuchunguza tuhuma hiyo ya matumizi ya zaidi ya Sh milioni 40 yaliyofanywa kwa maofisa hao.

Akizungumza na wanahabari jana, Mwenyekiti wa Talgwu wa wilaya hiyo, Andrea Mwandimbile alisema katika maadhimisho hayo yaliyofanyika Ilula, wilayani humo, wafanyakazi hao walikuwa wapate zawadi ya kati ya Sh 250,000 na Sh 200,000 kwa kuwa watendaji bora katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.Lakini walipewa bahasha tupu.

Akijibu malalamiko hayo, Kaimu Mkurugenzi huyo alisema; “kulikuwepo na tatizo dogo la mawasiliano lililochelewesha mchakato wa utoaji wa fedha kwa ajili ya kuwapa zawadi watumishi hao.”

Wampembe alisema mchakato wa kupata fedha hizo unaendelea kufanywa na wakati wowote kuanzia sasa watumishi hao watapewa haki yao

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...