Skip to main content

Mbaroni kwa ‘utapeli’ akijifanya mkuu CCP

Kilimanjaro linamshikilia mkazi wa eneo la Mwakilyambiti, kijiji cha Hungumalwa, wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, Joseph Maliuta (27) kwa tuhuma za kujipatia Sh milioni 11 kwa wizi wa mtandao baada ya kujiita Mkuu wa Chuo cha Polisi Moshi (CCP), Matanga Mbushi.

Mtuhumiwa huyo alifanikiwa kuiba fedha hizo kupitia mitandao ya simu za mkononi baada ya kuwarubuni wakazi wa kijiji cha Hungumalwa kwamba angewasaidia kuwapa nafasi watoto wao kujiunga na chuo cha Polisi Moshi.

Kamanda wa Polisi wa Kilimanjaro, Fulgence Ngonyani alisema tukio hilo lilitokea Mei 8 majira ya saa mchana katika kijiji hicho baada ya mtuhumiwa kusajili jina la mkuu wa chuo hicho katika simu yake kupitia huduma za kifedha.

Alisema mtuhumiwa alimfuata mmoja wa wakazi wa kijiji hicho, Ngeleja Shusha (42) na kumuuliza iwapo anahitaji kusaidia mtoto wake kuingia katika chuo cha Polisi Moshi, jambo ambalo mkazi huyo alikubali anahitaji msaada huo.

“Baada ya mazungumzo, Shusha ambaye ni mfanyabiashara, alisema ana watoto watatu wanaohitaji kuingia chuo cha Polisi ambapo wa kike ni mmoja na wa kiume wawili, ambapo alitakiwa kutangaza neema hiyo kwa wanakijiji wengine,” alisema.

Pamoja na Shusha lakini pia mtuhumiwa huyo alimtaka mkazi huyo kutafuta watu wengine wenye mahitaji kama yake ili waweze kusaidia watoto wao kujiunga na chuo cha Polisi kwa malipo ya Sh 250,000 kwa kila mtoto jambo ambalo lilitekelezwa na wanakijiji hao.

Alisema kutoka na udanganyifu huo, mkazi huyo alifanikiwa kukusanya kiasi cha Sh milioni 11 ambazo zote zilitumwa kwa mtuhumiwa ili aweze kutoa msaada waliohitaji.

Kamanda Ngonyani alisema baada ya Polisi kutapa taarifa za kufanyika kwa wizi huo iliweka mtego ambao ulisaidia kumnasa mtuhumiwa ambaye tayari amefikishwa mjini Moshi ili kufanyika kwa uchunguzi ili baadaye afikishwe mahakaman

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...