Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ameaga rasmi katika wizara hiyo na kujivunia kuweza kuwarudisha nchini maofisa na mabalozi wote waliostaafu nje ya nchi huku akiahidi kujaza nafasi za walioshika nafasi hizo kabla hajaondoka katika wizara hiyo.
Alisema hatua hiyo imewezeshwa baada ya wizara yake kupatiwa Sh bilioni 3.3 kwani kuna walioteuliwa miaka saba hadi nane, lakini hawajaenda katika vituo vya kazi kutokana na uhaba wa fedha, ambao ni mabalozi watano na maofisa 19.
Akizungumza katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo, Membe alisema pia watafanya mkutano wa mabalozi hivi karibuni baada ya kuwa kwa sasa wana uwezo wa kufanya kikao hicho, kwani walishindwa kufanya hivyo kwa muda mrefu.
Akiwaaga wafanyakazi hao, alisema kuwa kikao hicho ni cha mwisho, kwani kitakachokuja hatakuwa Waziri wa Mambo ya Nje na atakapokuwa ni siri ya Mungu, kwani atajaribu vitu vingine.
“Haitawezekana wala kutokea tena kuwa waziri wa mambo ya nje, lakini kwa jinsi wizara hii inavyopika viongozi, kwani asilimia 40 ya wafanyakazi wa Ikulu ni kutoka wizara hii, nikipata ajira popote nitaajiri kutoka wizara hii, kinachotakiwa ni kuombeana,” alisema.
Membe alisisitiza kuwa hakuna wizara inayotoa viongozi mbalimbali kama hiyo, kwani inapika viongozi, siyo wa diplomasia ya siasa na uchumi tu, bali viongozi wengine wa kada mbalimbali.
Alisema pamoja na matatizo ya kifedha waliyonayo katika wizara hiyo, wameweza kuzalisha viongozi wazuri akiwemo yeye, ambaye anatokea kwenye wizara hiyo, ambapo alisema wameongeza posho kwa wafanyakazi wa wizara hiyo wanaofanya kazi wakati wa ziada
Comments
Post a Comment