Skip to main content

Membe aaga wizarani kwake

Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ameaga rasmi katika wizara hiyo na kujivunia kuweza kuwarudisha nchini maofisa na mabalozi wote waliostaafu nje ya nchi huku akiahidi kujaza nafasi za walioshika nafasi hizo kabla hajaondoka katika wizara hiyo.

Alisema hatua hiyo imewezeshwa baada ya wizara yake kupatiwa Sh bilioni 3.3 kwani kuna walioteuliwa miaka saba hadi nane, lakini hawajaenda katika vituo vya kazi kutokana na uhaba wa fedha, ambao ni mabalozi watano na maofisa 19.

Akizungumza katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo, Membe alisema pia watafanya mkutano wa mabalozi hivi karibuni baada ya kuwa kwa sasa wana uwezo wa kufanya kikao hicho, kwani walishindwa kufanya hivyo kwa muda mrefu.

Akiwaaga wafanyakazi hao, alisema kuwa kikao hicho ni cha mwisho, kwani kitakachokuja hatakuwa Waziri wa Mambo ya Nje na atakapokuwa ni siri ya Mungu, kwani atajaribu vitu vingine.

“Haitawezekana wala kutokea tena kuwa waziri wa mambo ya nje, lakini kwa jinsi wizara hii inavyopika viongozi, kwani asilimia 40 ya wafanyakazi wa Ikulu ni kutoka wizara hii, nikipata ajira popote nitaajiri kutoka wizara hii, kinachotakiwa ni kuombeana,” alisema.

Membe alisisitiza kuwa hakuna wizara inayotoa viongozi mbalimbali kama hiyo, kwani inapika viongozi, siyo wa diplomasia ya siasa na uchumi tu, bali viongozi wengine wa kada mbalimbali.

Alisema pamoja na matatizo ya kifedha waliyonayo katika wizara hiyo, wameweza kuzalisha viongozi wazuri akiwemo yeye, ambaye anatokea kwenye wizara hiyo, ambapo alisema wameongeza posho kwa wafanyakazi wa wizara hiyo wanaofanya kazi wakati wa ziada

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...