Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Jakaya Kikwete ameshasaini miswada 9 katika ya 14 iliyopitishwa na bunge katika mkutano wake wa 19 ukiwemo wa sheria ya makosa ya mitandao pamoja na muswada wa sheria ya takwimu iliyozua utata.
Akitoa taarifa kuhusu kusainiwa kwa miswada hiyo leo Bungeni Spika wa Bunge Anna Makinda amesema miswada mitano iliyobaki atatolea ufafanuzi baada ya kupata kibali kutoka kwa Rais.
Makinda ametaja Miswada mingine iliyosainiwa ni pamoja na Muswada wa Sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa, Muswada wa Sheria ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Stakabadhi Ghalani, Muswada wa Sheria ya Kudhibiti Silaha, Muswada wa Sheria ya Miamala ya Kiektoniki pamoja na Muswada wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa.
Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania
Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati Mapinduzi hayo yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada ya tangazo la kupindulikwa kwake, Rais huyo alipanda ndege kurejea nchini kwake licha ya tangazo la kufungwa kwa mipaka yote na viwanja vya...
Comments
Post a Comment