Skip to main content

Mkurugenzi Mkuu Vodacom aliyejiuzulu Aula Qatar ......Mitandao Yahusisha Kujiuzulu Kwake na Kashfa ya Upotevu wa Bilioni 700 za Kitanzania

Aliyekuwa  Mkurugenzi  mkuu  wa  Vodacom  aliyejiuzulu hivi  karibuni  Rene Meza amepata shavu katika kampuni nyingine ya mawasiliano  nchini Qatar ijulikayo kama Ooredoo Mynmar kuwa Mwenyekiti  mtendaji  wa tawi la Mynmar.

Aidha, taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana  na kampuni hiyo imesema kwamba Rene Meza atachukua nafasi ya  Ross Cormack ambaye anatarajiwa kuachia nafasi hiyo mwaka huu.

Kwa mujibu wa mtandao wa Afrika Kusini umebanisha kwamba Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom amejiuzulu  ili kufanya kazi nyingine.

Hata hivyo mitandao ya kijamii  mbalimbali  nchini Tanzania imehusisha  kuondoka kwake  na kashfa ya upotevu wa takribani  bilioni 700 fedha za kitanzania ambazo ni sawa dola za Kimarekani  milioni 350.

Taarifa  hizo  zinaarifu  kuwa  bwana Meza alikuwa kwenye  ‘kitimoto’ cha maofisa wa juu wa Kampuni hiyo akihusishwa na kashfa ya kupokea dola milioni 5 kutoka kwa Mmiliki wa Shivacom,Tanil Somaiya ambaye  alimpa  ili  kumziba mdomo   kutokana  na  kashfa   ya  uzalishaji, usambazaji na uuzaji  wa  vocha  bandia  zilizokuwa  zinajulikana  kwa  jina  la  "Jero jero".

Rene Meza alijiunga na Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom mwaka 2011 akitokea kampuni ya Bhati Airtel Ltd ya nchini Kenya.

Ifuatayo  ni taarifa iliyotolewa na kampuni ya Ooredoo Mynmar ya nchini Qatar

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...