Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick, akikata utepe kufungua maonyesho ya uwekezaji katika majengo yajulikanayo kama Dar Property Expo kwenye ukumbi wa VIP wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, Jumamosi Mei 2, 2015. Makampuni na mabenki mbalimb ali yanashiriki kwenye maonyesho hayo
Maafisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakiwapatia maelezo wananchi kuhusu namna wanavyoweza kupata nyumba na jinsi walivyowekeza kwenye majengo waliotembelea banda la Mfuko huo
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick, akipatiwa maelezo na Afisa wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, anayeshughulikia uwekezaji katika majengo, Augustine K Paul, wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipotembelea banda la Mfuko huo mara baada ya kufungua maonyesho ya siku nne ya uwekezaji katika majengo (DAR property Expo), kwenye ukumbi wa VIP wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, Jumamosi Mei 2, 2015
Mkuu wa Mkoa akitembelea banda la Nevada Properties, kampuni inayojihusisha na ujenzi wa majengo
Mkuu wa mkoa akimsikilizaAfisa biashara mwandamizi wa kampuni nya Kilimani Industrial Automation Ltd, (KIAL), Shaban Issa, kuhusu mashine ya kumnyanyua fundi ujenzi kwenda juu wakati wa ujenzi wa majengo marefu ijulikanayo kama Aerial Work Platform (AWP-Machine), wakati alipotembelea banda hilo
Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania
Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati Mapinduzi hayo yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada ya tangazo la kupindulikwa kwake, Rais huyo alipanda ndege kurejea nchini kwake licha ya tangazo la kufungwa kwa mipaka yote na viwanja vya...
Comments
Post a Comment