Skip to main content

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba.

MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma.

Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA).

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema.

Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bunda, mkoani Mara.

Pia yuko Odeka Samson wa Musoma (Mara). Kutoka Dar es Salaam, Mukoba (Ilala) anawaongoza wagombea kutoka mkoa huo, wengine wakiwa Midelo Mathias wa Kinondoni, Rwebangira Anderson wa Temeke na Maguye Charles wa Mkoa wa Pwani.

Mkoa wa Morogoro una wagombea wawili ambao ni Asumbisye Frank na Senyagwa Daudi, kutoka Dodoma ni Ambakisye Fadhili na Iringa ina mgombea mmoja Seugali Luth Saida, wakati Mbeya imetoa mgombea kutoka Rungwe, Canon Mtewe Leonard. Wengine ni Christopher Banda kutoka Mtwara na Said Waninga kutoka Lindi.

Aidha, Arusha ambao ni mwenyeji wa Mkutano huo wa CWT ina mgombea mmoja tu, Laizer Miage anayetoka wilayani Karatu. Idadi kama hiyo, yaani wagombea 28, pia wanawania nafasi za Makamu wa Rais na katika kitengo hicho, wengi ni wale wanaotokea mkoa wa Dar es Salaam (5) na Kanda ya Ziwa (4).

Tisa wamejitokeza kuwania ukatibu mkuu na wengi ni kutoka Kanda ya Ziwa wakiwemo, Fredy Mbuguni, Nyamwero Bwire na Byarugaba Bandiho wote wa Mara, Zacharia Muganda wa Sengerema, Mwanza, na Edward Philipo wa Shinyanga.

Wengine ni Elisante Dyamyeku wa Morogoro, Yahya Msulwa wa Kinondoni, Dar es Salaam ambaye ni katibu Mkuu wa chama hicho na Meruma Wasato wa Kibaha, Pwani.

Wanaowania nafasi ya Naibu Katibu Mkuu, Ezekiel Oluoch na Mpumbe Joseph, wote kutoka Kinondoni Dar es Salaam. Wengine ni Kauka Akyoo na Augustino Daudi kutoka Hai, Kilimanjaro, Augustina Massawe wa Moshi, John Gadiye, Anthony Gamba, Mukangara James, na Wilson David hawa ni kutoka Mwanza.

Pia wamo Frank Chalamila wa Morogoro, Mayo Wilhelmon wa Manyara, Festo Moshi wa Mbeya, Prosper Mutungi, na Tangatya Santuce wa Dodoma, Michael Ndangwe wa Iringa, Shiku Peter, Marwa Mbeu wa Mara. Halafu Addallah Khalfani na Ismail A. Ismail wa Mtwara.

Wengine ni Kanyaiyangiro Evordius, Mathias Midelo na Fidelis Kisukilo kutoka Pwani, Lenda Majebera wa Tabora na Jairos Leonora wa Sumbawanga Rukwa. Pia wamo Raphael Joseph wa Geita na Simu Mussa wa Singida.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...