Skip to main content

Monday, May 4, 2015 Waziri Mkuu Aunda Kamati Kushughulikia Usafiri

Waziri Mkuu, Mizengo Peter Pinda ameunda kamati maalumu ya kudumu ya kusimamia Usafiri wa barabarani nchini ili kutatua changamoto zinazoikabali sekta ya Usafiri.

Katika kamati hiyo mwenyekiti wake atakuwa katibu mkuu wa wizara ya chukuzi, Katibu akiwa kamishna wa polisi barabarani na Mkurugenzi wa SUMATRA huku wajumbe wakiwa ni pamoja na katibu mkuu wizara ya kazi ya na ajira, katibu mkuu ujenzi, mwanasheria mkuu wa serikali na naibu katibu mkuu ofisi ya waziri mkuu.

Mkuu wa ratibu wa idara ya maafa toka ofisi ya waziri mkuu, mwenyekiti wa TABOA na TATOA, CHAKUA nao wanatakiwa kuanza kufanya vikao leo na kila mwezi watakutana kujadili na kutatua changamoto zote kasoro zile za kisheria ambazo zitapelekwa serikalini kwa mchakato zaidi wa kuzirekebisha.

Wakati huo huo umoja wa vyama vya madereva nchini Tanzania umesema hauna taarifa juu ya wao kutakiwa kukutana na waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda kwa ajili ya mazungumzo kama inavyozungumzwa na kusisitiza kuwa wao wataendelea na mgomo wao ulioanza leo mpaka masuala yao yatapofanyiwa kazi.

Akizungumza na East Africa Radio leo Makamu Mwenyekiti wa Muungano wa vyama vya Madereva Abdallah Lubala amesema kauli ya kuwa wamekubaliana kukutana na Mh. Pinda ni za kisiasa na hazina ukweli wowote hivyo wataendelea na mgomo wao.

Wakati huo huo mgomo huo ambao umetangazwa kwa nchi nzima athari zake zimejitokeza katika mikoa mingine tofauti ambapo madereva wa mabasi ya abiria wamegoma huku wasafiri wakitumia usafiri mbadala wa bajaji pamoja bodaboda.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi wa jiji la Mbeya, Arusha na Mwanza wamesema kuwa wanalazimika kutembea umbali mrefu kwenda makazini na wangine wakitumia gharama kubwa kutokana na vyombo hivyo wanavyotumia kupandisha bei za nauli kuliko kawaida

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...