Skip to main content

Mtanzania ateuliwa Mkurugenzi Mkuu Msaidizi WHO

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dk Margaret Chan amemteua Mtanzania, Dk Winnie Mpanju- Shumbusho kuwa Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa shirika hilo.

Uteuzi huo wa Dk Mpanju unaanza Juni mosi, mwaka huu na ulitangazwa wakati wa kikao cha Baraza la WHO lililofanyika Mei 18 hadi Mei 26, mwaka huu Geneva, Uswisi.

Kutokana na uteuzi huo, Dk Mpanju sasa ataongoza Kitengo cha WHO kinachoshughulikia Ukimwi, kifua kikuu, malaria na magonjwa yasiyopewa kipaumbele.

Atafanya kazi hiyo kwa kushirikiana na nchi husika katika kudhibiti magonjwa hayo, hivyo kutoa mchango katika maendeleo na mafanikio ya Malengo ya Milenia na Malengo Endelevu ya Maendeleo.

Dk Mpanju ana uzoefu wa zaidi ya miaka 30 katika nafasi za juu za uongozi wa masuala ya afya, afya ya jamii, ushirikiano wa kimataifa na elimu kwa ujumla.

Kabla ya uteuzi huo, Mpanju alikuwa Mkurugenzi katika ofisi ya Mkurugenzi Msaidizi wa WHO anayeshughulikia Ukimwi, kifua kikuu, malaria na magonjwa yasiyopewa kipaumbele Chini ya uongozi wake, WHO ilisaidia nchi zinazoendelea, hasa zile zinazotishiwa na magonjwa, kupata misaada ya zaidi ya dola za Marekani bilioni 10 kutoka Mfuko uitwao Global Fund, kugharimia programu za kitaifa za kupambana na Ukimwi, kifua kikuu na malaria, na programu za tiba na kinga za kuboresha afya ya uzazi, mama na mtoto.

Pia, Dk Mpanju amewahi kuwa Mkuurugenzi Mkuu wa Sekretatieti ya Masuala ya Afya ya Jumuiya ya Madola kwa ajili ya nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika. Ofisi za sekretarieti hiyo zipo Arusha, Tanzania.

Amewahi kuwa mjumbe wa bodi mbalimbali za kitaifa na kimataifa, ikiwemo Global Fund kwa ajili ya kupambana na Ukimwi, kifua kikuu na malaria na Bodi ya Mamlaka za Maji Mijini nchini Tanzania.

Dk Mpanju-Shumbusho ana Shahada ya Udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Shahada ya Uzamili katika Afya ya Jamii kutoka Chuo Kikuu cha Tulane, New Orleans, Marekani.

Pia ana Shahada ya Uzamili ya Udaktari kuhusu Watoto na Afya ya Watoto ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Dk Mpanju ameolewa na ana watot

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...