Skip to main content

Mtanzania ateuliwa Mkurugenzi Mkuu Msaidizi WHO

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dk Margaret Chan amemteua Mtanzania, Dk Winnie Mpanju- Shumbusho kuwa Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa shirika hilo.

Uteuzi huo wa Dk Mpanju unaanza Juni mosi, mwaka huu na ulitangazwa wakati wa kikao cha Baraza la WHO lililofanyika Mei 18 hadi Mei 26, mwaka huu Geneva, Uswisi.

Kutokana na uteuzi huo, Dk Mpanju sasa ataongoza Kitengo cha WHO kinachoshughulikia Ukimwi, kifua kikuu, malaria na magonjwa yasiyopewa kipaumbele.

Atafanya kazi hiyo kwa kushirikiana na nchi husika katika kudhibiti magonjwa hayo, hivyo kutoa mchango katika maendeleo na mafanikio ya Malengo ya Milenia na Malengo Endelevu ya Maendeleo.

Dk Mpanju ana uzoefu wa zaidi ya miaka 30 katika nafasi za juu za uongozi wa masuala ya afya, afya ya jamii, ushirikiano wa kimataifa na elimu kwa ujumla.

Kabla ya uteuzi huo, Mpanju alikuwa Mkurugenzi katika ofisi ya Mkurugenzi Msaidizi wa WHO anayeshughulikia Ukimwi, kifua kikuu, malaria na magonjwa yasiyopewa kipaumbele Chini ya uongozi wake, WHO ilisaidia nchi zinazoendelea, hasa zile zinazotishiwa na magonjwa, kupata misaada ya zaidi ya dola za Marekani bilioni 10 kutoka Mfuko uitwao Global Fund, kugharimia programu za kitaifa za kupambana na Ukimwi, kifua kikuu na malaria, na programu za tiba na kinga za kuboresha afya ya uzazi, mama na mtoto.

Pia, Dk Mpanju amewahi kuwa Mkuurugenzi Mkuu wa Sekretatieti ya Masuala ya Afya ya Jumuiya ya Madola kwa ajili ya nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika. Ofisi za sekretarieti hiyo zipo Arusha, Tanzania.

Amewahi kuwa mjumbe wa bodi mbalimbali za kitaifa na kimataifa, ikiwemo Global Fund kwa ajili ya kupambana na Ukimwi, kifua kikuu na malaria na Bodi ya Mamlaka za Maji Mijini nchini Tanzania.

Dk Mpanju-Shumbusho ana Shahada ya Udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Shahada ya Uzamili katika Afya ya Jamii kutoka Chuo Kikuu cha Tulane, New Orleans, Marekani.

Pia ana Shahada ya Uzamili ya Udaktari kuhusu Watoto na Afya ya Watoto ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Dk Mpanju ameolewa na ana watot

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.