Skip to main content

Muhimbili Yakumbwa na Uhaba wa Damu

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) imekumbwa na uhaba wa damu hali ambayo imeulazimu uongozi wa hospitali hiyo kuomba msaada wa dharura kwa Serikali na watu binafsi.

Uongozi huo pia umewaomba Watanzania, mashirika ya umma, makampuni  na watu binafsi kujitokeza kusaidia kuchangia damu  kuokoa maisha ya wagonjwa  wanaopelekwa katika hospitali hiyo.

Taarifa iliyotolewa jana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Aminiel Aligaesha, ilieleza kuwa kwa siku hospitali hiyo huhitaji wastani wa chupa za damu 70 hadi 100 kwa siku.

Alisema hali hiyo inachangiwa na ongezeko la mahitaji ya damu ambayo hutumika zaidi hasa kwa wagonjwa wa dharura, kina mama wajawazito, wagonjwa waliofanyiwa upasuaji, watoto  na wagonjwa wa saratani.

“Kila mgonjwa wa upasuaji wa moyo anahitaji kiasi cha chupa tano mpaka sita za damu. Matumizi haya yanafanyika kabla, wakati na baada ya kufanyiwa upasuaji,” alisema Aligaesha.

Alisema kwa wiki hii wamelazimika kufungua kambi maalumu za Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka nchi mbalimbali ambao wanashirikiana na madaktari wa hapa nchini kufanya upasuaji wa moyo, kati ya wagonjwa watano hadi sita kwa siku.

“Wagonjwa wa moyo pekee huitaji chupa 30 hadi 36 kwa siku. Kambi hizi zimeanza mapema Aprili mwaka huu na tunatarajia kuwa nazo katika  miezi mitatu ijayo kama njia ya kuwafanya madaktari hawa waendelee kuja na kufanya upasuaji wa moyo kwa ufanisi  ambako damu huhitajika zaidi,” alisema Eligaesha.

Alisema hospitali hiyo ya taifa hutegemea kupata damu kutoka vyanzo vikuu viwili ambavyo ni ndani ya hospitali na  Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS).

“Makusanyo ya damu kutoka vyanzo vya ndani ni kati ya chupa 20 hadi 40 kwa siku  huku matumizi yakiwa chupa 70 hadi 100.

“Mathalani kuanzia Aprili 17 mwaka huu hatukuweza kupata damu hata chupa moja kutoka Mpango wa Taifa Damu Salama hali iliyosababisha upungufu mkubwa wa damu hospitalini hapa ikilinganishwa na mahitaji,” alisema.

Alisema Hospitali ya Taifa Muhimbili imejipanga kupitia kitengo chake cha Uchangiaji Damu kilichopo Maabara Kuu kuwapokea watu watakaojitokeza kuchangia damu.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...