Skip to main content

Polisi 3 kortini kwa upotevu wa SMG 8

Published on Wednesday, 13 May 2015 00:29
Written by Lucas Raphael, Tabora
Hits: 120

ASKARI Polisi watatu wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) mkoani Tabora, wamefikishwa mahakamani, akiwemo mkuu wa kikosi hicho, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Bhoke Julius Bruno.

Wote wanatuhumiwa kwa upotevu wa bunduki nane aina ya SMG, mali ya Jeshi la Polisi. Wengine waliopandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Tabora, Issa Magori ni Koplo Idd Abdalah na Mwinyi Gonga, wote wa kikosi cha FFU, Tabora.

Akiwasomea mashitaka, Wakili wa Serikali, Juma Masanja aliiambia mahakama hiyo kuwa watuhumiwa wote watatu wanakabiliwa na shitaka moja la kutochukua tahadhari stahiki katika utunzaji wa silaha.

Alidai watuhumiwa hao, walitenda kosa hilo kati ya Aprili na Mei mwaka jana wakiwa waajiriwa wa Jeshi la Polisi, Kikosi cha Kutuliza Ghasia mkoani Tabora.

Wakili Masanja alidai watuhumiwa wakiwa Kikosi cha FFU Tabora kwa pamoja, walishindwa kutumia njia za kiusalama katika utunzaji wa silaha na matokeo yake bunduki nane aina ya SMG, zikaingia katika mikono ya watu ambao hawajaidhinishwa kwenye umiliki wake.

Watuhumiwa wote watatu walikana shitaka hilo na walinyimwa dhamana baada ya Wakili wa Serikali kupinga wasipewe kwa maelezo kwamba kuwepo kwao nje, kutaingilia upelelezi wa upatikanaji wa silaha hizo.

Kutokana na ombi hilo la serikali, Mahakama iliamuru watuhumiwa warudishwe mahabusu hadi Mei 21 mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa tena

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...