Skip to main content

Polisi Wapambana na Wananchi Njombe

JESHI la Polisi jana lililazimika kutumia zaidi ya saa 5.00 kupambana na wananchi waliokuwa wakiandamana bila kibali wakitaka kuchukua maiti ya mmoja wa wakazi wa Njombe aliyedaiwa kuuawa kwa kupigwa risasi na askari wa jeshi hilo wakati wa msako wa wanywa pombe.

Mtu huyo   inaelezwa alifariki dunia  juzi na mwili wake kuhifadhiwa katika  Hospitali ya  Kibena.

Inaelezwa wananchi hao walikuwa wakiandamana  kuuchukua mwili wa marehemu huyo na kuupeleka polisi.

Wakizungumzaia tukio hilo, baadhi ya wananchi walisema   juzi saa 3.00 usiku  polisi walivamia   kilabu  cha  pombe  kilichopo  Zenge Mtaa wa Kambarage na  kuwakamata  watu zaidi ya 20  waliokuwa wakilewa kilabuni hapo.

Baada ya  wananchi hao  kukamatwa  wakiwamo  wahudumu,  inadaiwa  polisi hao waliokuwa wamevalia ‘kininja’ waliwapiga  raia  walioonyesha  kukaidi agizo la  kutaka kutoa fedha walizokuwa nazo kama faini ya  kunywa  pombe   usiku huo.

Kijana mmoja,   Bashiri Mwalongo, ambaye alikuwa akitaka akitaka kutoka mlangoni alijikuta akipigwa na  kitu  kinachosadikika kuwa   risasi  tumboni  na  kufa papo hapo.

Inaelezwa kuwa  Polisi wa Kikosi  cha Kutuliza Ghasia (FFU), jana  walilazimika kuwatawanya waandamanaji hao kwa mabomu ya machozi.

Wananchi hao  walikuwa wanataka kwenda kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Dk. Rehema Nchimbi,  kuwasilisha malalamiko yao.

Vurugu hizo   zilisambaa na kusababisha baadhi ya shughuli za jamii yakiwamo  maduka mjini Njombe kufungwa.

Mashuhuda walisema vurugu hizo zilisababisha barabata Kuu ya Njombe - Ruvuma na  Iringa ya  Njombe - Iringa na Njombe  - Makete  kufungwa na  waandamanaji hao ambao  walichoma  matairi ya magari katikati ya barabara.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, alishindwa  kuzungumza na waandishi wa habari   kutoa ufafanuzi wa vurugu hizo kwa vile alichukua muda mrefu kwa kuwa katika  kikao na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...