Published on Thursday, 14 May 2015 21:04
Written by Theopista Nsanzugwanko
Hits: 10
MAMLAKA ya Udhibiti wa Umma (PPRA) imesema sheria ya manunuzi ya umma siyo mbaya kama inavyolalamikiwa na wadau mbalimbali, bali tatizo ni uelewa wa sheria hiyo.
Mwenyekiti wa bodi wa PPRA, Balozi Matern Lumbanga alisema hayo jana wakati akizungumzia maadhimisho ya miaka kumi ya mamlaka hiyo.
Maadhimisho hayo yatafanyika kuanzia Mei 18 hadi 21 mwaka huu yenye kaulimbiu ya miaka kumi ya PPRA tumethubutu, tumeweza,tushirikiane kuboresha zaidi manunuzi ya umma.
Alisema katika miaka yote hiyo wamekuwa wakiboresha mifumo, ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya sheria hiyo lakini bado yanafanyika makosa,huku yakiwepo madai ya sheria ni mbaya.
“Tukidhibiti manunuzi ambayo ni nusu ya bajeti nzima ya serikali tunadhibiti upotevu wa fedha za serikali na nchi itapiga hatua ambapo PPRA tumekuwa tukitoa mafunzo kufafanua sheria hiyo na kanuni zake kwa lengo la kuimarisha utendaji, huku tukishirikiana na Takukuru kudhibiti vitendo vya rushwa, ”alisema Lumbanga.
Akizungumzia maadhimisho hayo, Balozi Lumbanga alisema yataanza Mei 18 mwaka huu kwa warsha maalumu ya wadau wa habari yatakayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee na uzinduzi utafanyika siku inayofuata na Waziri wa Fedha Saada Mkuya.
Comments
Post a Comment