Skip to main content

PPRA wasema sheria ya manunuzi iko sawa

Published on Thursday, 14 May 2015 21:04
Written by Theopista Nsanzugwanko
Hits: 10

MAMLAKA ya Udhibiti wa Umma (PPRA) imesema sheria ya manunuzi ya umma siyo mbaya kama inavyolalamikiwa na wadau mbalimbali, bali tatizo ni uelewa wa sheria hiyo.

Mwenyekiti wa bodi wa PPRA, Balozi Matern Lumbanga alisema hayo jana wakati akizungumzia maadhimisho ya miaka kumi ya mamlaka hiyo.

Maadhimisho hayo yatafanyika kuanzia Mei 18 hadi 21 mwaka huu yenye kaulimbiu ya miaka kumi ya PPRA tumethubutu, tumeweza,tushirikiane kuboresha zaidi manunuzi ya umma.

Alisema katika miaka yote hiyo wamekuwa wakiboresha mifumo, ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya sheria hiyo lakini bado yanafanyika makosa,huku yakiwepo madai ya sheria ni mbaya.

“Tukidhibiti manunuzi ambayo ni nusu ya bajeti nzima ya serikali tunadhibiti upotevu wa fedha za serikali na nchi itapiga hatua ambapo PPRA tumekuwa tukitoa mafunzo kufafanua sheria hiyo na kanuni zake kwa lengo la kuimarisha utendaji, huku tukishirikiana na Takukuru kudhibiti vitendo vya rushwa, ”alisema Lumbanga.

Akizungumzia maadhimisho hayo, Balozi Lumbanga alisema yataanza Mei 18 mwaka huu kwa warsha maalumu ya wadau wa habari yatakayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee na uzinduzi utafanyika siku inayofuata na Waziri wa Fedha Saada Mkuya.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...