Skip to main content

Raia wa Kenya anaswa akivunja ATM Arusha

Published on Tuesday, 05 May 2015 00:39
Written by John Mhala, Arusha
Hits: 68

MTU mmoja aliyetambulika kwa jina la Annuary Ally, raia wa nchi jirani ya Kenya ametiwa mbaroni na polisi baada ya kukutwa akivunja mashine ya kutolea fedha (ATM) ya Benki ya Barclays, Tawi la Stendi Kuu ya mabasi jijini hapa.

Kwa mujibu wa Ofisa Mikopo wa benki hiyo, Regina Kitali mtuhumiwa huyo alifika katika benki hiyo saa 5:15 asubuhi jana na kuingia katika mashine ya ATM kwa lengo la kutoa fedha.

Lakini baada ya dakika chache walisikia mtikisiko usiokuwa wa kawaida katika mashine hiyo na kumlazimu mmoja wa wafanyakazi wenzake kutoka nje kwenda kuangilia ni kitu gani.

Alisema baada ya mfanyakazi huyo kuingia ndani ya chumba hicho alimkuta Ally akiwa anajaribu kung’oa mashine hiyo ili apachike mashine maalumu aliyokuwa nayo kwa lengo la kuchukua fedha zilizokuwa ndani ya ATM hiyo.

Alisema baada ya kuona hali hiyo alimuuliza Ally kuna tatizo gani na kutaka kujua kama anahitaji msaada, lakini mtuhumiwa huyo alimjibu kuwa anataka kutoa fedha na alipotakiwa kupewa msaada alijifanya mbabe kwa kutaka kumtoa nje mfanyakazi huyo wa benki.

“Kufuatia hali hiyo mwenzetu alitoka nje mara moja na kubonyeza kengele ya tahadhari kuomba msaada kutoka kampuni ya ulinzi inayolinda katika tawi hili huku wengine tukipiga simu kuomba msaada wa polisi,” alisema.

Kwa mujibu wa Regina wakati mtuhumiwa akiendelea kung’oa mashine hiyo polisi wa kikosi cha FFU walifika eneo hilo na ndipo mtuhumiwa alipotoka nje na kuwaponyoka polisi na kuanza kukimbia kwa lengo la kutoroka.

Alisema walianza kupiga kelele za kuomba msaada ambapo raia wema walijitokeza na kuanza kumkimbiza mtuhumiwa huyo kwa kushirikana na polisi na kufanikiwa kumkamata katika eneo la benki ya NBC tawi la Meru huku akiwa na vitambulisho vingi vya aina mbalimbali pamoja na mashine hiyo maalumu.

Baada ya mtuhumiwa huyo kutiwa mbaroni alipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi kwa mahojiano zaidi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Mmoja wa wapiga debe wa stendi kuu ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alisema mtuhumiwa huyo alionekana kama abiria stendi tangu majira ya saa moja asubuhi akirandaranda karibu na ATM hiyo kama abiria aliyekuwa amekwama usafiri kutokana na mgomo wa mabasi ulionza tangu alfajiri.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas hakuweza kupatikana kuzungumzia tukio hilo kwani alikuwa nje ya ofisi kikazi na simu yake ya kiganjani ilikuwa inaita bila majibu.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...