Skip to main content

Raia wa Kenya anaswa akivunja ATM Arusha

Published on Tuesday, 05 May 2015 00:39
Written by John Mhala, Arusha
Hits: 68

MTU mmoja aliyetambulika kwa jina la Annuary Ally, raia wa nchi jirani ya Kenya ametiwa mbaroni na polisi baada ya kukutwa akivunja mashine ya kutolea fedha (ATM) ya Benki ya Barclays, Tawi la Stendi Kuu ya mabasi jijini hapa.

Kwa mujibu wa Ofisa Mikopo wa benki hiyo, Regina Kitali mtuhumiwa huyo alifika katika benki hiyo saa 5:15 asubuhi jana na kuingia katika mashine ya ATM kwa lengo la kutoa fedha.

Lakini baada ya dakika chache walisikia mtikisiko usiokuwa wa kawaida katika mashine hiyo na kumlazimu mmoja wa wafanyakazi wenzake kutoka nje kwenda kuangilia ni kitu gani.

Alisema baada ya mfanyakazi huyo kuingia ndani ya chumba hicho alimkuta Ally akiwa anajaribu kung’oa mashine hiyo ili apachike mashine maalumu aliyokuwa nayo kwa lengo la kuchukua fedha zilizokuwa ndani ya ATM hiyo.

Alisema baada ya kuona hali hiyo alimuuliza Ally kuna tatizo gani na kutaka kujua kama anahitaji msaada, lakini mtuhumiwa huyo alimjibu kuwa anataka kutoa fedha na alipotakiwa kupewa msaada alijifanya mbabe kwa kutaka kumtoa nje mfanyakazi huyo wa benki.

“Kufuatia hali hiyo mwenzetu alitoka nje mara moja na kubonyeza kengele ya tahadhari kuomba msaada kutoka kampuni ya ulinzi inayolinda katika tawi hili huku wengine tukipiga simu kuomba msaada wa polisi,” alisema.

Kwa mujibu wa Regina wakati mtuhumiwa akiendelea kung’oa mashine hiyo polisi wa kikosi cha FFU walifika eneo hilo na ndipo mtuhumiwa alipotoka nje na kuwaponyoka polisi na kuanza kukimbia kwa lengo la kutoroka.

Alisema walianza kupiga kelele za kuomba msaada ambapo raia wema walijitokeza na kuanza kumkimbiza mtuhumiwa huyo kwa kushirikana na polisi na kufanikiwa kumkamata katika eneo la benki ya NBC tawi la Meru huku akiwa na vitambulisho vingi vya aina mbalimbali pamoja na mashine hiyo maalumu.

Baada ya mtuhumiwa huyo kutiwa mbaroni alipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi kwa mahojiano zaidi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Mmoja wa wapiga debe wa stendi kuu ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alisema mtuhumiwa huyo alionekana kama abiria stendi tangu majira ya saa moja asubuhi akirandaranda karibu na ATM hiyo kama abiria aliyekuwa amekwama usafiri kutokana na mgomo wa mabasi ulionza tangu alfajiri.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas hakuweza kupatikana kuzungumzia tukio hilo kwani alikuwa nje ya ofisi kikazi na simu yake ya kiganjani ilikuwa inaita bila majibu.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...