mwanzo
Biashara
Biashara
Serikali yarudisha neema kwa wakulima Bumbuli
Share bookmark Print Email Rating
‘Mambo yote yako tayari. Kilichokuwa kinasubiriwa ni kibali ambacho kimekwisha kutolewa na Rais Kikwete.’ January Makamba, Mbunge Bumbuli
Na Raisa Said, Mwananchi
Posted Jumatatu,Mei4 2015 saa 12:2 PM
Kwa ufupi
Ni baada ya kuridhia kutoa fedha kwa ajili ya kifufua kiwanda cha chai
SHARE THIS STORY
0
inShare
Bumbuli. Mgogoro kati ya wakulima wa chai Bumbuli na mwekezaji wa Kiwanda cha Chai Mponde, umefikia tamati baada ya Serikali kuridhia kutoa fedha kwa ajili ya kufufua kiwanda hicho ambacho kilikuwa kimefungwa kwa muda wa miaka miwili baada ya wakulima kugomea kuuza majani mabichi ya chai katika kiwanda hicho.
Akizungumzia hatua ya kufufua uzalishaji wa kiwanda hicho kilichopo Mponde katika Halmashauri ya Bumbuli, Mbunge wa Jimbo hilo, January Makamba alisema, Serikali imeridhia kutoa Sh4 bilioni ambazo ni gharama za kulipa madeni ya malimbikizo ya mishahara ya wafanyakazi, madeni ya malipo ya wakulima, ukarabati na mtaji wa kuanzia kuendesha shughuli za uzalishaji.
Mtaji huo utatumika pamoja na mambo mengine, kununua kuni za kwanza kwa ajili ya kiwanda na kukarabati magari ambayo alieleza kuwa baadhi yake vipuri vilitolewa.
Makamba ambaye yupo katika ziara ya kutembelea jimbo lake la Bumbuli, alisema Serikali ilituma wataalamu kufanya tathmini yenye lengo la kutambua gharama za ufufuaji wa kiwanda hicho kilichokuwa kikiendeshwa na Chama cha Wakulima wa Chai cha Usambara (Utega) na mwekezaji ambaye ni Kampuni ya Chai ya Lushoto katika miaka ya 2000.
“Hivi sasa ni Hazina ndiyo inayosubiriwa itoe fedha hizo kwa ajili ya kukarabati kiwanda na gharama nyingine,” alisema Makamba wakati akizungumza na wakulima katika Kijiji cha Kweminyasa, katika Kata ya Mponde.
Taarifa za kutolewa kwa kibali cha fedha za kufufua kiwanda hicho zimepokelewa kwa furaha na wakulima ambao hata hivyo waliiomba Serikali kuongeza kasi ya utoaji wa fedha ili waondokane na matatizo ya kiuchumi na kijamii yaliyotokana na kufungwa kwa kiwanda hicho.
Akizungumzia uamuzi huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli, Beatrice Msomisi alisema, Serikali imewapa matumaini ya kuongeza mapato ya ndani yaliyodorora kutokana na kufungwa kwa kiwanda hicho.
Comments
Post a Comment