Skip to main content

Shuka yamuua mwendesha pikipiki Kiteto

MKAZI wa Kijiji cha Ndeleta kilichopo wilayani Kiteto, Mkoa wa Manyara, Saria Kidali (47), amefariki dunia baada ya kunyongwa na shuka alilokuwa amejifunika wakati akiendesha pikipiki.

Tukio hilo la aina yake lilitokea jana asubuhi wakati Kidali alipokuwa akitoka shambani kwake Nadosoiti.

Kabla ya kifo hicho, shuka ya mwendesha pikipiki huyo ilinasa kwenye tairi ya nyuma na shuka hiyo kumbana shingo Kidali hadi alipopoteza maisha baada ya kudondoka chini.

Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Manyara, Christopher Fuime, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuitaja pikipiki iliyomuua Kidali kuwa ni aina ya Toyo yenye namba za usajili T613 BEB.

“Pikipiki hiyo inasemekana ni mali ya marehemu na taarifa za awali zinaonyesha chanzo cha kifo hicho ni shuka alilokuwa amevaa kwani lilijizungusha kwenye tairi na kumnyonga shingo,” alisema Kamanda Fuime.

Pamoja na hayo, alitoa wito kwa waendesha pikipiki kuchukua tahadhari wakati wote ili kuepukana na ajali zinazoweza kuepukika.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo, waliitonya MPEKUZI kwamba, walipata taarifa za tukio hilo kutoka kwa abiria wa basi moja la abiria lililokuwa likitoka wilayani Kiteto kuelekea Arusha.

Mmoja wa mashuhuda hao aliyejitambulisha kwa jina la Lazaro Gidion, alisema marehemu Kidali hakukutwa na majeraha yoyote ingawa shingo yake ilikuwa imezungukwa na shuka.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Ndaleta lilikotokea tukio hilo, Ijumaa Bakari, aliwataka wananchi wa eneo hilo kutovaa shuka wakati wanaendesha pikipiki kwa kuwa zinaweza kuhatarisha maisha yao

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...