Skip to main content

Simba yasaka kocha Serbia, Sweden

MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Klabu ya Simba Zacharia Hans Poppe, amesema zoezi la kumtamfuta mrithi wa kocha Goran Kopunovic tayari limeanza na nchi ambazo wamezilenga ni Serbia, Sweden na Uingereza.

Hans Poppe alisema jana kuwa bado hawajamaliza mazungumzo na kocha wao wa sasa Kopunovic, lakini wana wasiwasi huenda wasifikie muafaka kutokana na kocha huyo kupata tamaa na kuhitaji kiasi kikubwa cha fedha tofauti na kile cha awali.

Hata hivyo habari za ndani ambazo gazeti hili inazo ni kwamba Simba imeshafanya maamuzi ya kuachana na Kopunovic baada ya kutaka kulipwa Shilingi milioni 100 kwa mkataba usiozidi mwaka mmoja.

Hans Poppe, alisema wameamua kufanya hivyo lengo ni kujiweka tayari kwa chochote kitakachotokea kuhusiana na kocha huyo kama ikishindikana kuendelea naye wawe na kazi nyepesi ya kumalizana na kocha mpya ambaye ndiyo wanamtafuta hivi sasa.

“Lengo letu ni kuanza mapema maandalizi kwa ajili ya msimu ujao pamoja na michuano ya Kombe la Kagame kwa hiyo lazima tujiandae kwa kila kitu ndiyo sababu kwa sasa tupo katika mazungumzo na makocha sita ambao mmoja wao anaweza kuifundisha timu yetu kama mazungumzo na Kopunovic yatashindikana,”alisema Hans Poppe.

Hans Poppe amewataka mashabiki wa timu hiyo kuwa watulivu wakati uongozi wao ukiendelea kupambana kuwaletea kocha atakaye ibadili timu yao na kuipa mafanikio makubwa msimu ujao ikiwemo kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara.

Kopunovic aliwasili nchini mwishoni mwa Desemba mwaka jana na kuingia mkataba wa miezi sita kuifundisha Simba baada ya Mzambia Patrick Phiri kutupiwa virago.

Simba iliamua kuachana na Phiri baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa timu. Kopunovic aliikuta Simba ikiwa nafasi ya 12 kwenye msimamo na kuiongoza mpaka kumaliza ligi nafasi ya tatu.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...