Skip to main content

Sunday, May 3, 2015 Madereva bodaboda hatarini kupungukiwa nguvu za kiume

WAFANYABIASHARA wadogo na waendesha bodaboda wanaofanya biashara zao kwenye njia kubwa za kusafirishia umeme wapo hatarini kupungukiwa nguvu za kiume.

Kutokana na kuwepo wengi kwenye njia hizo kubwa za kusafirishia umeme, wametahadharishwa kutoendelea kufanya biashara kwenye maeneo hayo.

Hayo yalibainishwa jana na Ofisa Mahusiano Msaidizi huduma kwa wateja wa Tanesco Mwanza, Haji Bwegege wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya uzinduzi wa maonyesho ya siku ya wafanyakazi uliofanywa na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo kwenye viwanja vya Furahisha, jijini hapa.

“Tumekuwa tukiielimisha jamii mara kwa mara kutofanya biashara kwenye njia ya umeme mkubwa unaopita kutokana na madhara wanayoweza kuyapata na hii ya kupungukiwa nguvu za kiume ni moja ya madhara ambayo yanaweza kuwapata hivyo wachukue tahadhari mapema,” alisema.

Aliyataja madhara mengine kuwa pamoja na mwili kupoteza nguvu kutokana na mionzi hivyo wananchi kutakiwa kuishi umbali wa mita 30 kila upande pamoja na mjamzito kuharibu mimba.

Akizungumzia suala la ‘Vishoka’, Bwegege aliwataka wananchi wasikubali kuuziwa fomu majumbani kwani fomu za kuomba kuunganishiwa umeme hutolewa ofisini tu ama pale maofisa wao wanapotembelea vijijini wakiwa na vitambulisho na kutoa risiti.

“Mnatambua kuwa miradi ya umeme vijijini inaendelea ya Wakala wa Umeme Vijijini (REA) na Electricity five (F5) hivyo vishoka kutumia nafasi hiyo kuwarubuni wananchi ambapo wamekuwa wakifika vijijini na kuwauzia fomu kati ya Sh 60,000 na 100,000 wakati bei halisi ya fomu ni Sh 5,900 tu,”alisema.

Alisema vishoka hao wamekuwa wakijitokeza katika maeneo ya vijijini ambapo miradi hiyo imekuwa ikiendelea na kwamba kama Tanesco wamekuwa wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi kwa kufanya mikutano ya hadhara na kuwataka wananchi wajiandikishe kwenye ofisi za serikali za vijiji.

Bwegege alisema chini ya miradi ya wakala wa umeme vijijini, wananchi wanaozungukwa na mradi hutozwa Sh 27,000 kama gharama ya kuungiwa umeme.

Alisema wameshiriki katika maonesho hayo ili kutoa elimu kwa jamii juu ya shughuli zao na kwamba huduma zote zinazotolewa ofisini zinatolewa uwanjani hapo

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...