Skip to main content

Taasisi ya mifupa MOI yapata msaada

TAASISI ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) imepokea msaada wa kifaa cha kufanyia upasuaji chenye thamani ya Sh milioni 700 kutoka Chuo Kikuu cha Tiba cha Weill Cornell cha nchini Marekani.

Msaada huo umetolewa na chuo hicho ikiwa ni sehemu ya ushirikiano kati ya taasisi ya MOI.

Akizungumza jana Meneja Ustawi na Uhusiano wa taasisi hiyo, Almas Jumaa, alisema kifaa hicho kitatumika kufanya upasuaji wa ubongo, uti wa mgongo, mishipa ya fahamu na mifupa.

Alisema kifaa hicho kimeingia chumba cha upasuaji jana tayari kwa matumizi ya upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Chuo cha Weil Cornell.

“Wataalamu kutoka Chuo cha Cornell watatoa mafunzo ya vitendo kwa wataalamu wa taasisi ya MOI kwa kutoa huduma ya matibabu na upasuaji kwa wagonjwa kwa kutumia kifaa hicho.

“Tunatarajia kufanya upasuaji kwa wagonjwa 24 kwa muda wa siku tatu na upasuaji utakaofanyika ni wa kesi kubwa ambazo awali tulikuwa tunapeleka wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu,” alisema Jumaa.

Alisema msaada walioupata ni kutokana na ushirikiano mzuri kati ya taasisi hiyo na chuo hicho hali itakayosaidia kuongeza ufanisi wa utoaji huduma na uwezo wa kuhudumia wagonjwa wengi.

Alisema wagonjwa wenye matatizo ya mishipa ya fahamu wamekuwa wakiongezeka kila siku na kwa sasa wanapokea wagonjwa 35 mpaka 40 kwa siku.

Alisema kwa sasa taasisi hiyo ina vifaa vya kutosha na ushirikiano na Chuo cha Cornell utaongeza ujuzi katika matumizi ya vifaa hivyo na kutoa huduma bora.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...