Skip to main content

Tanesco kuja na viwango vipya

Published on Thursday, 14 May 2015 00:07
Written by Sifa Lubasi, Dodoma
Hits: 783

SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) linakusudia kupanga viwango vipya vya malipo ya umeme vitakavyotoa unafuu kwa taasisi hiyo na wadau wake endapo vyombo vinavyohusika, ikiwamo EWURA vitaidhinisha.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Idara ya Mipango Mikakati kutoka Tanesco Makao Makuu, Patrick Sankara katika Mkutano ulioandaliwa na Tanesco Makao Makuu na kufanyika Dodoma mkoani hapa.

Mkutano huo ni mwendelezo wa mikutano ya shirika hilo na wateja wake wenye lengo la kupata maoni ya watumiaji wake na kuzijua changamoto zitakazokuwepo baada ya Tanesco, kuanzia mpango wa kugawa viwango vya bei ya umeme kulingana na muda wa matumizi.

Alisema wale watakaokubadili muda wa matumizi watapatiwa punguzo maalumu kwenye viwango vyao.

Alisema matumizi ya umeme kwa sasa hupanda ghafla kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 4:00 usiku na kusababisha msukumo wa umeme kutoka katika vyanzo vyake kupungua na kusababisha Tanesco kuwasha mashine za ziada kufidia mzigo huo.

Akiwasilisha mada katika mkutano huo iliyohusu “Viwango vya muda wa matumizi ya Umeme”, Sankara alisema kutokana mahitaji hayo Tanesco inaingia gharama kubwa kuhakikisha inakidhi matakwa ya wateja wake.

“Gharama zote za kufidia matumizi haya ya ziada ni za Tanesco hivyo tunadhamiria kuja na mpango wa kuwashawishi wateja wakubwa kuhamisha muda wa matumizi yao kutoka saa za jioni na kuja muda wa asubuhi na mchana ambapo matumizi si makubwa sana,” alisema.

Akichangia katika majadiliano hayo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Chiku Gallawa aliishauri Tanesco Mkoa wa Dodoma, kubuni utaratibu mpya wa kuwahudumia wateja wake ili kupunguza malalamiko na kukuza mahusiano mema.

Naye Kaimu Meneja wa Tanesco Kanda ya Kati, Joel Kuandika aliuambia mkutano huo kuwa wamepokea mapendekezo ya wateja hao na kuahidi kuyashughulikia ipasavyo.

Wakichangia mada hizo, baadhi ya watumiaji hao wakubwa walikubaliana na Tanesco kuhusu utaratibu mpya, lakini baadhi yao walionesha wasiwasi endapo Tanesco itaweza kusimamia utekelezaji wake kwa haki na umakini

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...