Skip to main content

Tuhuma za wanaume Rombo zamfadhaisha mbunge wao

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini.Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini.

MADAI ya wanawake wa wilaya ya Rombo, Kilimanjaro, kukodi wanaume kutoka nchini Kenya, baada ya kukosa huduma za ndoa kutoka kwa waume zao kwa muda mrefu, kutokana na ulevi wa gongo uliopindukia, zimemfadhaisha Mbunge wao, Joseph Selasini (Chadema).

Mbunge huyo amefikia hatua ya kusema kuwa familia yake na wananchi wa huko, wamefadhaika na kuingiwa na wasiwasi kuwa huenda wenzi wao katika ndoa zao ikiwemo ya mbunge, si waaminifu.

Selasini alisema hayo jana, alipokuwa akiuliza swali kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambapo alisema ingawa hali hiyo imewafadhaisha, lakini alitetea utengenezaji wa pombe za kienyeji, ikiwemo pombe haramu ya gongo.

Katika utetezi huo, Selasini alitaka Serikali iangalie namna ya kusaidia uboreshwaji wa pombe za kienyeji, kwa kuwa kipato chake kimekuwa kikisaidia ada za watoto, kujikimu na kuongeza kipato cha familia.

Akijibu swali hilo, Pinda alisema kwa namna Selasini anavyozungumza, huenda anatetea suala la kuhalalisha pombe haramu aina ya gongo, na kama ndio hiyo Serikali itaendelea kupiga vita utengenezaji na matumizi ya pombe hiyo kwa sababu viwango vyake havipimiki.

“Mheshimiwa Selasini, kwa maelezo yako utakuwa unazungumzia gongo, sasa hii ni pombe haramu na Serikali inaendelea kuipiga vita kwa kuwa viwango vyake havipimiki.

“Lakini huenda kwa siku zijazo, jambo hili linaweza kuangaliwa na kiwanda cha Konyagi kuhusu namna ya kuiboresha kwa sababu hata Konyagi ni jamii ya gongo, lakini inapimika na haina madhara makubwa kwa watumiaji,” alisema Pinda.

Hata hivyo, katika swali la nyongeza la mbunge huyo, alimtaka Waziri Mkuu kukanusha tuhuma za Mkuu wa Wilaya ya Rombo, Lembrice Kipuyo alizotoa wiki iliyopita akidai kuwa wanawake wa wilaya hiyo, wanakodisha wanaume kutoka nchi jirani ya Kenya kwa ajili ya kuwahudumia mahitaji ya kimwili, kwa kuwa waume zao wameshindwa kutokana na ulevi uliopindukia.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu, tunaomba kauli ya serikali kuhusu jambo hili, na mkanushe taarifa hizo kwani zimeleta mfadhaiko kwenye familia na hata familia yangu, wanandoa wana wasiwasi kwamba wenza wao wanatoka nje ya ndoa, lakini pia kauli hiyo ni ya kudhalilisha wananchi wa Rombo”, alisema Selasini.

Akijibu swali hilo, Pinda alisema hajasikia tuhuma hizo ;na kwamba kama zimetolewa na Mkuu huyo wa Wilaya ni vyema aliyetoa, azikanushe mwenyewe kwa kuwa ndiye anayejua alizitoa katika mazingira gani na wapi.

Aidha, alisema ni vyema apewe muda wa kulifahamu jambo hilo ;na kusema ataiagiza Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuangalia jambo hilo kama Mkuu huyo wa Wilaya alichokisema, sio sahihi ili hatua nyingine zifuate.

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila alimuuliza Waziri Mkuu atoe kauli ya serikali kuhusu kukwama kutolewa kwa fedha za wahisani kwenye bajeti ya serikali, kutokana na wahisani hao kugoma kwa madai ya sakata ya akaunti ya Escrow.

Hatua hiyo imesababisha fedha za Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC) awamu ya pili, hazijasainiwa na kusema Waziri wa Fedha awali alilidanganya Bunge kuwa fedha hizo zimeshasainiwa na kutaka serikali kutoa kauli juu ya kauli ya uongo ya waziri huyo.

Akijibu hoja hizo, Waziri Mkuu alisema suala la Waziri wa Fedha kusema uongo sio lake, bali la Bunge na hivyo Bunge ndilo lenye jukumu ya kuchukua hatua, ikiwa waziri huyo alilidanganya Bunge na kwamba tatizo la ufinyu wa bajeti ya nchi, halitokani tu na wahisani kusitisha fedha zao kwa sababu ya sakata la Escrow, bali ni la muda mrefu.

“Nijibu hili la ufinyu wa bajeti, sio kweli kwamba sakata la Escrow ndio chanzo kikuu, miaka mitatu sasa na zaidi wahisani wameendelea kusuasua kutoa fedha zao, ndio maana serikali imeamua sasa kujikita zaidi kuangalia vyanzo vya ndani vya mapato zaidi kuliko kuwategemea hao”, alisema Pinda.

Kuhusu kauli ya Waziri wa Fedha kulidanganya Bunge juu ya kusainiwa kwa awamu ya pili ya fedha za MCC, kutokana na sakata la Escrow, Pinda alisema waziri husika atalitolea ufafanuzi bungeni.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...