Skip to main content

Uchaguzi Yanga Julai

KLABU ya Yanga inatarajiwa kufanya uchaguzi Mkuu Julai 12 mwaka huu ambapo nafasi za Mwenyekiti , Makamu Mwenyekiti na Wajumbe zitawaniwa.

Awali uchaguzi huo ulikuwa ufanyike mwaka jana lakini baadhi ya wanachama walimwomba Mwenyekiti anayemaliza muda wake Yusuf Manji kuendelea kuwania tena nafasi hiyo kitu ambacho kilimlazimu kuwaomba wanachama hao asogeze mbele uchaguzi ili apate muda wa kufikiria ombi lao.

Akizungumza na gazeti hili Katibu Mkuu wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga Francis Kaswahili, aliwataka watu mbalimbali wenye mapenzi ya dhati na klabu hiyo kujitokeza kuwania nafasi hizo kwa lengo la kuipa mafanikio zaidi klabu hiyo.

“Jambo hili ni la kikatiba na wala halina mjadala, tunataka Yanga iwe na viongozi ambao watatokana na utashi wa Wanayanga ni matumaini ya Kamati ya Uchaguzi kwamba hapatatoka mtu mwingine wa kutaka kuvunja misingi ya Katiba,”alisema Kaswahili.

Alisema lengo la kutangaza tarehe ya uchaguzi mapema ni kutaka kupata viongozi wapya ambao watapata muda mzuri wa kuiandaa timu kwa ajili ya kutetea ubingwa wao wa bara msimu ujao na kufanya vizuri katika michuano ya Ligi ya Mabingwa ambayo mwakani.

Kaswahili alisema fomu za kuwania uongozi kwenye klabu yao zitaanza kutolewa keshokutwa kwa kuzingatia taratibu na kanuni ambazo zitawekwa kwa nia njema ya kuhakikisha klabu yao inapata viongozi bora.

Mara ya mwisho Yanga ilifanya Uchaguzi wake Mkuu Julai 18,2010 ambapo Lloyd Nchunga alichaguliwa kuwa Mwenyekiti na Delvis Mosha alichaguliwa katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti huku wajumbe wakiwa ni Charles Mgondo, Ally Mayay, Mzee Yusuf na Theonest Rutashobolwa, Titus Ossoro, Sara Ramadhani, Mohamed Binda na Salum Rupia.

Lakini baadhi ya viongozi hao walijiuzulu nyadhifa zao na hivyo ikalazimika kufanyika uchaguzi mdogo Julai 15,2012 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee na Manji alichaguliwa kuwa Mwenyekiti na Clement Sanga akichaguliwa kama Makamu Mwenyekiti na nafasi za Wajumbe wakachaguliwa Aaron, Nyanda, George Manyama, Abdallah Bin Kleb na Valentine Katabalo

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...