Skip to main content

UKIUKAJI WA SHERIA: Selcom yazuiwa kuuza Luku >

Posted Friday, May 1, 2015 | by- Suzan Mwillo, Mwananchi
UKIUKAJI WA SHERIA: Selcom yazuiwa kuuza Luku

>Serikali imefuta mkataba wake na kampuni ya Selcom iliyokuwa inauza umeme wa Luku kwa kile
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene.
ADVERTISEMENT

Dar es Salaam. Serikali imefuta mkataba wake na kampuni ya Selcom iliyokuwa inauza umeme wa Luku kwa kile kilichodaiwa kuwa ni ubabaishaji katika kutoa huduma hiyo.

Pia kampuni hiyo, ambayo imekuwa ikinunua umeme wa jumla kutoka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) imesitishiwa mkataba huo kutokana na kukiuka sheria na taratibu za ulipaji wa kodi.

Hata hivyo, mkurugenzi mtendaji wa Selcom, Sameer Hirji hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo.

“Siwezi kuzungumzia chochote kuhusu hilo (mkataba). Tutakuwa na mkutano na waandishi wa habari kesho (leo),” alisema.

Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene aliitaka Tanesco kufuata uamuzi wa Serikali kwa kuwa Selcom imekuwa ikilalamikiwa na wateja kuwa na matatizo ya kiufundi kila wanaponunua umeme, hasa ifikikapo mwisho wa mwezi.

“Hatuwezi kuendelea kuvumilia hali hii kwa sababu hafai. Hiyo nafasi tumeiondoa, tunawapa wengine. Utendaji wao mbovu na umekuwa ukisababisha wananchi kukosa umeme.

“Mteja anafika kwa wakala kununua umeme, anaambiwa hakuna, tunarekebisha mitambo yetu,” alisema.
ADVERTISEMENT

Selcom na Maxcom ndiyo kampuni pekee zilizoshinda zabuni za kuuza nishati hiyo na kuingia mkataba na Tanesco wa kununua umeme wa jumla na kuuza kwa rejareja. Hata hivyo imeelezwa kuwa Maxcom imekuwa ikifanya vizuri kuliko Selcom.

Simbachawene, ambaye amechukua nafasi iliyoachwa na Profesa Sospeter Muhongo, alisema pia wameichukulia hatua za kisheria kampuni hiyo kutokana na kukuika taratibu za kulipa kodi.

“Kwa mujibu wa sheria za kodi hawawezi kuendelea kutoa huduma na hili wala halina athari zozote kwa sababu wao ndiyo wamevunja sheria... naomba wananchi wanunue umeme katika vituo vya Maxcom hadi pale tutakapopata muuzaji mwingine,” alisema

Mkurugenzi wa Tanesco, Felchesmi Mramba alisema kabla ya kuchukua uamuzi huo walipokea barua kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiwataka wasitishe mkataba wao na Selcom.

“Ukiachilia mbali malalamiko yaliyokuwa yanatolewa na wananchi. TRA walituambia tusifanye kazi na hao jamaa huku wakiwatuhumu kwa kugushi nyaraka na kukiuka taratibu za kulipa kodi.

“Kwa hiyo tulishatekeleza hilo tangu jana na sasa kampuni pekee tunayofanyanayo baishara ya hiyo ni Maxcom.”

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo alisema:  “Kwa mujibu wa sheria zetu, haturuhusiwi kumjadili mlipa kodi na mtu ambaye siyo muhusika. Haya ni mambo binafsi.”

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...