Skip to main content

UN waunga mkono kazi ya Kikwete

Nyalandu amewaonya watendaji wa wizara yake wanaojifanya miunguwatu na kushindwa kufuata taratibu za kazi na kunyanyasa wananchi, kuwa atawaondoa mchana kweupe.

Alisema ana mamlaka ya kufanya hivyo muda wowote na kwamba kila bora na makini ni yule mwadilifu na anayejali na kushughulikia matatizo ya wananchi na si kunyanyasa ama vinginevyo.

Aliwataka wananchi hususan jamii ya wafugaji kumfikishia taarifa sahihi kuhusu wahifadhi kwenye mapori ya akiba wanaowatoza faini kubwa ama kuagiza mifugo ipigwe risasi ili ashughulike nao kwani ni kinyume cha sheria.

“Hakuna mtendaji wa wizara yangu aliyepo juu ya sheria…unyanyasaji na rushwa ni makosa ya jinai na kamwe sitakubali yawepo ndani ya taasisi za wizara ninayoiongoza. Kila mtendaji afuate sheria na anayekiuka nina mamlaka ya kumuondoa muda wowote,” alisema Nyalandu wakati alipozungumza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na wafugaji kutoka mikoa yote nchini, uliofanyika juzi jioni mjini Lamadi mkoani Simiyu.

Kauli hiyo inatokana na wafugaji kulalamika kuonewa na baadhi ya watendaji, hususan wahifadhi na askari wa wanyamapori. Katibu Mkuu wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Magembe Makoye, alisema matukio ya wafugaji kunyanyaswa yameshika kasi na wahusika wakubwa ni wahifadhi na askari wa wanyamapori.

Alisema matukio ya ng’ombe kukamatwa na kupigwa risasi ndani na nje ya hifadhi, yamezidi kushika kasi huku watendaji wakijigamba hakuna wa kuwakataza wala kuwawajibisha kwa ukatili huo.

Kutokana na malalamiko hayo, Nyalandu amepiga marufuku wahifadhi na askari wa wanyamapori kujichukulia sheria mkononi na kuheshimu haki za wengine.

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani, amewaonya watendaji wanaopiga marufuku ama kukwamisha usafirishaji wa mifugo kwenda nchi ya nchi, kuacha tabia hiyo kwani wanahujumu uchumi.

Alisema mifugo inayosafirishwa nje ya nchi na ambayo imefuata taratibu, ikiwa ni pamoja na mfanyabiashara kuwa na vibali halali vya serikali, haipaswi kuzuiwa na kupiga marufuku tabia hiyo.

Amewaonya baadhi ya wafanyabiashara wanaosafirisha mifugo kwenda nje kwa kutumia njia za panya na wengine kutumia vibali vya kughushi arobaini yao imefika na wajiandae kupanda mahakamani kwa kuhujumu uchumi.

Dk Kamani alikuwa akizungumza kwenye mkutano huo wa hadhara, uliowakutanisha wafugaji kutoka mikoa yote nchini, uliohudhuriwa na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira, Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Erasto Mbwilo.

Mkutano huo ulikuwa ukifikisha kilio cha muda mrefu cha wafugaji kuhusiana na maeneo ya malisho na manyanyaso, wanayodai kufanyiwa na wahifadhi kwenye mapori ya akiba na askari wa wanyamapori.

Alisema mifugo inayosafirishwa nje ya nchi inakuza uchumi wa taifa na wafugaji kwa ujumla na kwamba, tabia za baadhi ya watendaji kukwamisha kwa sababu zao binafsi ili kupata chochote hazikubaliki.

Pia alitumia fursa hiyo kuagiza kuwa asilimia 10 ya mapato ya minada ya mifugo itengwe kwa ajili ya kuboresha sekta ya mifugo nchini ikiwa ni pamoja na maeneo ya malisho na maji kwa wafugaji.

Awali, katika risala yao kwa Nyalandu, wafugaji hao walilalamikia kunyanyaswa na wahifadhi, ikiwa pamoja na kuuawa kwa kupigwa risasi wao na mifugo wao.

Walidai kutokana na manyanyaso hayo wamegeuzwa kuwa mashine za kutolea pesa (ATM) na wahifadhi wakiwemo askari wanayamapori wanapowakamata na kuwatoza kuwatoza faini kubwa kuliko kawaida na fedha hizo huishia mifukoni mwao

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...