MKAZI wa Mbezi Juu David Oturo, amesema yupo katika maandalizi ya kuwasafirisha watoto wake wawili waliopoteza maisha Mei 17 mwaka huu baada ya kupigwa shoti ya Umeme katika Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo katika Viwanja vya Tanganyika Peakas Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na jana baba mzazi wa watoto hao Oturo alisema kuwa anatarajia kuwasafirisha watoto wake ambao ni Sarah David(10) na Goodluck David(04) leo au kesho kuelekea Mkoani Musoma kwa ajili ya mazishi.
Alisema kifo cha watoto wake ni cha utata kutokana na kwamba watoto walikuwa ni wengi katika eneo hilo lakini ameshangaa watoto wake wote wawili kupigwa na shoti ya umeme na wote baada ya hapo walipelekwa katika Hospitali ya TMJ na kuhamishiwa katika Hospitali ya Mwananyamala lakini wote walipoteza maisha.
Akizungumzia suala la ushiriki wa kanisa katika msiba huo alisema kuwa Askofu Gwajima pamoja na waumini wake wanafika nyumbani kwake lakini hawajashiriki kitu chochote.
“Kwa sasa nipo katika maandalizi ya kuwasafirisha watoto wangu kwenda Musoma kwa ajili ya mazishi, ingawaje katika maandalizi yangu Askofu Gwajima na waumini wake hawajatoa kitu chochote kwa ajili yamaandalizi ya safari hii.
“Mimi ninachong’ang’ana ni kuhakikisha kuwa wanangu ninawasafirisha kwenda kuwapumnzisha nyumbani kwetu nilipozaliwa ambako ni Musoma na si vinginevyo,” alisema Oturo.
Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima alipotafutwa kuzungumzia swala hilo simu yake iliita bila kupokelewa na wakati mwingine ilikuwa ilikuwa haipatikani kabisa.
Pamoja na jitihada za kupiga simu kwa askofu huyo kugongwa mwamba, lakini ilisikika miito ya nyimbo pamoja na mahubiri mbalimbali katika simu yake.
Moja ya muito huo ulisikika ukisema “Biblia ni njia kwa waliopotea, Biblia ni njia kwa waliokata tama, Biblia ni uponyaji kwa wagonjwa, Bibilia ni faraja kwa walio na dhiki,” yalisikika maneno hayo.
Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania
Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati Mapinduzi hayo yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada ya tangazo la kupindulikwa kwake, Rais huyo alipanda ndege kurejea nchini kwake licha ya tangazo la kufungwa kwa mipaka yote na viwanja vya...
Comments
Post a Comment