Skip to main content

Vifo vya Watoto Kanisani kwa Gwajima Bado ni Utata.

MKAZI wa Mbezi Juu David Oturo, amesema yupo katika maandalizi ya kuwasafirisha watoto wake wawili  waliopoteza maisha  Mei 17 mwaka huu  baada ya kupigwa shoti ya Umeme   katika Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo katika Viwanja vya Tanganyika Peakas Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na jana baba mzazi wa watoto hao Oturo alisema kuwa anatarajia kuwasafirisha watoto wake ambao ni Sarah David(10) na Goodluck David(04) leo au kesho kuelekea Mkoani Musoma kwa ajili ya mazishi.

Alisema kifo cha watoto wake ni cha utata kutokana na kwamba watoto walikuwa ni wengi katika eneo hilo lakini ameshangaa watoto wake wote wawili kupigwa  na shoti ya umeme na wote baada ya hapo walipelekwa katika Hospitali ya TMJ na kuhamishiwa katika Hospitali ya Mwananyamala lakini wote walipoteza maisha.

Akizungumzia suala la ushiriki wa kanisa katika msiba huo alisema kuwa Askofu Gwajima pamoja na waumini wake wanafika nyumbani kwake lakini hawajashiriki kitu chochote.

“Kwa sasa nipo katika maandalizi ya kuwasafirisha watoto wangu kwenda Musoma kwa ajili ya mazishi, ingawaje katika maandalizi yangu  Askofu Gwajima na waumini wake hawajatoa kitu chochote kwa ajili yamaandalizi ya safari hii.

“Mimi ninachong’ang’ana  ni kuhakikisha kuwa wanangu ninawasafirisha kwenda kuwapumnzisha nyumbani kwetu nilipozaliwa ambako ni Musoma na si vinginevyo,” alisema  Oturo.

Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima alipotafutwa kuzungumzia swala hilo simu yake iliita bila kupokelewa na wakati mwingine ilikuwa ilikuwa haipatikani kabisa.

Pamoja na jitihada za kupiga simu kwa askofu huyo kugongwa mwamba, lakini ilisikika  miito ya nyimbo pamoja na mahubiri  mbalimbali katika simu yake.

Moja ya muito huo ulisikika ukisema  “Biblia ni njia kwa waliopotea, Biblia ni njia kwa waliokata tama, Biblia ni uponyaji kwa wagonjwa, Bibilia ni faraja kwa walio na dhiki,” yalisikika maneno hayo.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...