Msanii wa muziki wa Bongo Flavor Diamond Platinumz(wa pili kutoka kushoto) na balozi wa Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom Tanzania akiwaonyesha program hiyo waandishi wa habari(hawamo pichani) wakati wa uzinduzi wake uliozinduliwa wakati wa Zari white party iliyofanyika mlimani city jijini Dar es Salaam jana.App hiyo inawaletea wateja burudani ya muziki kiganjani.Wengine katika picha ni Maofisa Mawasiliano wa kampuni hiyo,Abigail Ambweni(wa kwanza kushoto) na Glory Mtui.
Ofisa Mawasiliano na Matukio wa Vodacom Tanzania, Abigail Ambweni(kulia)akihojiwa na mtangazaji wa clouds TV wakati wa uzinduzi wa program ya Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom Tanzani.Uzinduzi huo ulifanyika wakati wa Zari white party iliyofanyika mlimani city jijini Dar es Salaam jana.App hiyo inawaletea wateja burudani ya muziki kiganjani.
Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(katikati)akimsikiliza jambo Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platinumz(kulia)na balozi wa Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi(mobile app)ya Vodacom Tanzania iliyozinduliwa jana wakati wa Zari white party iliyofanyika mlimani city jijini Dar es Salaam jana.
Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania
Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati Mapinduzi hayo yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada ya tangazo la kupindulikwa kwake, Rais huyo alipanda ndege kurejea nchini kwake licha ya tangazo la kufungwa kwa mipaka yote na viwanja vya...
Comments
Post a Comment