majukwaa yasiyo rasmi na kuhoji kipolisi mwanachama mmoja mmoja anayetuhumiwa kukosa, ni kichocheo cha uvunjifu wa amani, hivyo ikemewe, imeelezwa.
Mtaalamu wa masuala ya utatuzi wa migogoro ya kisiasa, Gharib Galant, aliyepewa kazi na Shirika la Kimataifa la Maendeleo (UNDP), atafiti na kuishauri Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, juu ya njia bora za kutatua migogoro ya vyama vya siasa, ndiye aliyesema hivyo Dar es Salaam jana.
Akizungumza kwenye mkutano wa mashauriano kati ya vyama 22 vya siasa nchini, taasisi mbalimbali, wadau wengine wa siasa na Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa, kuhusu njia sahihi ya kusimamia na kuendesha kwa amani siasa za vyama vingi, katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu, Galant alisema, utatuzi wa migogoro unahitaji haki na uwazi.
Kwa mujibu wake, mwanachama anayetuhumiwa kukosa ndani ya chama, anapaswa kupewa nafasi ya kujieleza katika vikao rasmi apate hakiyake ya kujitetea na kutetewa pindi inapobidi, na si kuchukuliwa sehemu na wachache kwa maelezo ya kuhojiwa.
“Inapotokea mwanachama amepelekwa katika eneo fulani na kufanyiwa mambo yasiyostahili kwa taratibu zisizo rasmi nani atafahamu kuwa ametendewa haki au la? kila mmoja anaweza akatoka huko na kudai jambo lake...”.
“Hali hiyo inaweza kusababisha kuvunjika kwa amani ndani ya chama husika, mashabiki wa mwanachama anayekuwa amehojiwa na kudai kutotendewa haki, pamoja na makundi mengine ya jamii ambayo, kwa njia moja au nyingine yanakuwa yameguswa.
Mgogoro kama huo unapoibuka, athari yake inaweza kutingisha amani ya nchi,”alisema. Ingawa mtaalamu huyo hakukitaja chama chochote kuwa na tabia hiyo, Februari mwaka huu, Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) kilituhumiwa kuwatumia walinzi wake, kumuadabisha aliyekuwa mlinzi wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa, Khalid Kagenzi kwa madai ya kutaka kumuua kiongozi huyo.
Kagenzi alilalamika kuwa walinzi hao walimkamata na kumfungia ndani ya chumba kimoja mali ya chama hicho, wakamtesa kwa kumpiga wakati wakimhoji kuhusu tuhuma hizo za kutaka kumuua Dk Slaa.
Pamoja na kuishauri ofisi hiyo ya Msajili wa vyama ikemee mapema hali hiyo, Galant alisema unapofanyika utatuzi wa migogoro ni lazima wahusika washirikishwe kwa ridhaa yao, wapewe nafasi sawa ya kujieleza bila kuwepo upendeleo kwa chama au kundi lolote.
Namna nyingine iliyotajwa na Galant kuwa ni bora katika kutatua migogoro ya vyama vya siasa au chama na wanachama wake ni ya kulipa Baraza la vyama vya siasa nafasi yake ya kutekeleza wajibu huo, badala ya kuikimbiza kwa Msajili au Mahakamani.
Katika hili, Galant alisema, “Ninashauri endapo Baraza hilo litashindwa kuwakutanisha wahusika wa mgogoro, au kuona kuwa mgogoro ni mkubwa unaoweza kuvuruga amani hivyo kusababisha uchaguzi mkuu na majukumu mengine makubwa katika nchi yasifanyike kwa wakati, litafute usaidizi wa wataalamu wa kutatua migogoro wanaokubalika ili wafanye kazi hiyo”.
Aliongeza kuwa kabla ya kuanza kupanga kushughulikia migogoro ni vizuri ukafanywa utafiti wa aina ya migogoro, ili kujua ni njia zipi zitumike kuimaliza, badala ya kukimbilia kuisuluhisha kwa sababu njia nyingine zinaweza kuizidisha.
Katika hatua nyingine, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula alipendekeza Baraza la Vyama vya Siasa nchini liwezeshwe kifedha lifanikishe kazi zake, ikiwa ni pamoja na kujisambaza katika ngazi zote, zikiwemo za chini.
Comments
Post a Comment