Skip to main content

Wabunge Dar wajipanga kumkwamisha Magufuli

MBUNGE wa Temeke, Abbas Mtemvu (CCM), amesema wabunge wa Dar es Salaam wanasubiri makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Ujenzi ili waikwamishe, kutokana na kutotimiza ahadi ilizotoa kwa mkoa huo.

Akizungumza jana katika mjadala wa makadirio ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mtemvu alisema wabunge wote wa Dar es Salaam wanamsubiri Waziri wa Uchukuzi, Dk John Magufuli wamkwamishe kwa kuwa ahadi zake zimegeuka nyimbo.

Alisema Dk Magufuli alipokabidhiwa wizara hiyo, alisema amegundua dawa ya msongamano katika mji huo, lakini sasa anakaribia kumaliza muda wake msongamano huo umeongezeka, badala ya kupungua.

Alitoa mfano wa ahadi ya ujenzi wa barabara za Juu na kufafanua kuwa ahadi hiyo kila mara imekuwa wimbo kuhusu upembuzi yakinifu, huku msongamano ukizidi kuongezeka.

Mtemvu aliwaomba wabunge wote kwa kuwa sehemu kubwa wana makazi katika jiji hilo, kushirikiana na wabunge wa Dar es Salaam kupata kauli moja ya Bunge kuhusu msongamano kwa kuwa na wao wanaathirika.

Kwa mujibu wa Mtemvu, karibu kila mbunge akisimama anazungumzia jimbo lake, wakati ana makazi katika jiji hilo ambalo pamoja na kuchangia karibu asilimia 75 ya pato la Taifa, lakini linasumbuliwa na msongamano mkubwa wa magari.

Aliomba Serikali pia itenge posho na vifaa kwa askari wa Usalama Barabarani wa jiji hilo, ambao wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana na hasa wakati wa mvua.

Alimpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kufanya ziara kutembelea waathirika wa mafuriko, yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Mbunge wa Viti Maalumu, Zarina Madabida (CCM), aliitaka Serikali itenge fedha kwa ajili ya marekebisho ya barabara zilizoharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha.

Alibainisha kuwa wabunge na madiwani wa Dar es Salaam, waliamua kujenga barabara za pete au za pembezoni hafifu za lami badala ya za changarawe, ili kuepuka kufanya marekebisho ya mara kwa mara.

Uamuzi huo kwa mujibu wa Madabida, ulisababisha msongamano wa magari kupungua kwa kuwa magari mengi yalitumia barabara hizo zilizokuwa zikipitika.

Hata hivyo, alisema kuwa mafuriko yaliyokumba jiji hilo yameharibu barabara hizo hafifu za lami na msongamano unaoonekana, umetokana na watu kurejea katika barabara kuu kwa kuogopa kuharibika kwa barabara hizo za pete

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...