Skip to main content

Walimu 1,200 kukutana na JK

wanatarajiwa kukutana na Rais Jakaya Kikwete mjini Arusha, wiki ijayo wakati kiongozi huyo wa nchi atakapokuwa akifungua rasmi mkutano wao mkuu wa mwaka kitaifa.

“Tunatarajia kuwa walimu wapatao 1,200 kutoka mikoa 25 na wilaya 153 za Tanzania Bara watakutana na Rais Kikwete katika eneo la Ngurdoto, wilayani Meru, mkoani Arusha.

Mkutano huo Mkuu wa Chama cha Walimu Taifa (CWT) utafanyika kati ya Mei 26 hadi 28, mwaka huu,” alisema Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Arusha, Juvin Buruya na kuongeza: “Walimu wote Tanzania watawakilishwa vema kwenye mkutano huo ambapo tutatumia fursa ya uwepo wa Rais Kikwete kumuomba amalizie ahadi zake kadhaa alizowaahidi wakufunzi hao kabla hajastaafu rasmi,” alisema.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo wa CWT mkoani Arusha, walimu watakaojumuika kwenye mkutano mkuu, watatumia fursa hiyo kumuaga rasmi mke wa Rais, Mama Salma Kikwete ambaye pia ni mwalimu.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CWT, Ezekiah Oluoch alisema chama hicho kimekuwa kikipata ushirikiano mzuri kutoka serikali ya awamu ya nne, na kwamba wanatarajia uhusiano huo mzuri kuendelea hata katika serikali ijayo ya awamu ya tano.

Oluoch alisema nchi sita zinatarajiwa kuhudhuria mkutano huo ambazo ni Uganda, Kenya, Denmark, Rwanda na Ghana, ambapo pia viongozi wastaafu wa CWT taifa pamoja na wawakilishi kutoka visiwa vya Zanzibar watakuwepo.

“Malengo makuu ya mkutano mkuu wa CWT taifa ni pamoja na kujadili taarifa za kazi ya chama na taarifa za mapato na matumizi pamoja na kupitia mpango mkakati wa miaka mitano 2015-2020,” aliongeza Naibu Katibu Mkuu.

CWT pia itafanya uchaguzi wa viongozi wa chama hicho kitaifa Mei 28, mwaka huu na tayari wagombea wapatao 452 wamejitokeza kuwania nafasi mbalimbali za CWT.

Nafasi hizo ni pamoja na Urais wa CWT, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mweka Hazina wa taifa, wawakilishi wa makundi maalumu yakiwemo yale ya walimu wanawake, walimu wenye ulemavu, walimu vijana pamoja na wadhamini wa chama.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...