Skip to main content

Walimu 1,200 kukutana na JK

wanatarajiwa kukutana na Rais Jakaya Kikwete mjini Arusha, wiki ijayo wakati kiongozi huyo wa nchi atakapokuwa akifungua rasmi mkutano wao mkuu wa mwaka kitaifa.

“Tunatarajia kuwa walimu wapatao 1,200 kutoka mikoa 25 na wilaya 153 za Tanzania Bara watakutana na Rais Kikwete katika eneo la Ngurdoto, wilayani Meru, mkoani Arusha.

Mkutano huo Mkuu wa Chama cha Walimu Taifa (CWT) utafanyika kati ya Mei 26 hadi 28, mwaka huu,” alisema Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Arusha, Juvin Buruya na kuongeza: “Walimu wote Tanzania watawakilishwa vema kwenye mkutano huo ambapo tutatumia fursa ya uwepo wa Rais Kikwete kumuomba amalizie ahadi zake kadhaa alizowaahidi wakufunzi hao kabla hajastaafu rasmi,” alisema.

Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo wa CWT mkoani Arusha, walimu watakaojumuika kwenye mkutano mkuu, watatumia fursa hiyo kumuaga rasmi mke wa Rais, Mama Salma Kikwete ambaye pia ni mwalimu.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CWT, Ezekiah Oluoch alisema chama hicho kimekuwa kikipata ushirikiano mzuri kutoka serikali ya awamu ya nne, na kwamba wanatarajia uhusiano huo mzuri kuendelea hata katika serikali ijayo ya awamu ya tano.

Oluoch alisema nchi sita zinatarajiwa kuhudhuria mkutano huo ambazo ni Uganda, Kenya, Denmark, Rwanda na Ghana, ambapo pia viongozi wastaafu wa CWT taifa pamoja na wawakilishi kutoka visiwa vya Zanzibar watakuwepo.

“Malengo makuu ya mkutano mkuu wa CWT taifa ni pamoja na kujadili taarifa za kazi ya chama na taarifa za mapato na matumizi pamoja na kupitia mpango mkakati wa miaka mitano 2015-2020,” aliongeza Naibu Katibu Mkuu.

CWT pia itafanya uchaguzi wa viongozi wa chama hicho kitaifa Mei 28, mwaka huu na tayari wagombea wapatao 452 wamejitokeza kuwania nafasi mbalimbali za CWT.

Nafasi hizo ni pamoja na Urais wa CWT, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mweka Hazina wa taifa, wawakilishi wa makundi maalumu yakiwemo yale ya walimu wanawake, walimu wenye ulemavu, walimu vijana pamoja na wadhamini wa chama.

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.