Skip to main content

‘Walimu jiepusheni na mambo ya ovyo’

NAIBU Waziri wa Elimu, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Kassim Majaliwa amewataka walimu nchini kujiepusha na mambo yanayochangia kukiuka misingi ya haki za binadamu na maadili mema.

“Mwalimu ni kioo cha jamii kuweni raia wema, chukieni maovu na kuweni mfano bora kwa jamii kwa kauli na matendo ili jamii ijifunze kutoka kwenu,” alisema Majaliwa.

Alisema hayo jana mjini hapa wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya haki za binadamu kwa walimu wa shule za sekondari, wakaguzi wa shule na wakufunzi wa vyuo vya ualimu kutoka mikoa ya Dodoma, Singida na Manyara.

Mafunzo hayo yamedhaminiwa na Shirika la Mipango ya Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP). Alisema ni jambo jema kama walimu watakuwa mfano wa kuigwa katika jamii na kuwa mabalozi wema na watetezi wa haki za binadamu, hususan watoto na watu wenye ulemavu kwa imani na vitendo na hatimaye kuongeza tija kazini.

“Baadhi ya walimu wamekuwa wakifanya kazi bila kuzingatia maadili ya kazi zao, kuendekeza rushwa, kutoa huduma zisizokidhi matarajio ya wananchi na hivyo kusababisha malalamiko ya wananchi dhidi ya serikali,” alisema.

Alisema ipo haja kubwa ya kueneza elimu ya haki za binadamu katika jamii ili haki hizo ambazo zimeainishwa katika katika ya nchi, sheria mbalimbali na mikataba ya haki za binadamu.

Naibu Waziri alisema katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na matukio mengi ya ya uvunjifu wa haki za binadamu ikiwemo ukatili dhidi ya watoto, vurugu na migomo katika shule na vyuo na matukio mbalimbali ya uhalifu yakiwemo wananchi kujichukulia sheria mkononi dhidi ya watuhumiwa wa uhalifu.

Alisema matukio mengine ni ukatili dhidi ya wanawake mauaji ya walemavu wa ngozi na vikongwe na ajali za barabarani matukio ambayo yanaashiria kuna uelewa mdogo dhidi ya haki za binadamu.

Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na utawala bora, Dk Kelvin Mandopi alisema tume hiyo iko katika utekelezaji wa mpango kazi wa kitaifa wa haki za binadamu wa mwaka 2013 hadi 2017 kwa lengo la kukuza na kulinda haki za binadamu nchini.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa UNDP, Godfyey Mbisa alisema lengo la programu hiyo ni kurahisisha ufundishaji wa haki za binadamu na kuzipa uzito unaostahili.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...