Skip to main content

Wananchi Sengerema Wampa BARAKA Ngeleja Kugombea Urais.......Wasema Jina Lake Likikatwa Arudi Agombee Ubunge

WAKAZI wa Vijiji vya Nyabila na Sigu, Jimbo la Sengerema, mkoani Mwanza, wamemuomba Mbunge wao, Bw. William Ngeleja kuwania nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Wamesema kama jina lake litakwama kupitishwa ndani ya chama, watamchagua kwa mara nyingine ili aendelee kuwa mbunge wao kwa kipindi cha miaka mitano kutokana na utendaji wake mzuri wa kazi.

Wakazi hao waliyasema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kijiji cha Nyabila, baada ya Bw. Ngeleja kuzindua miradi miwili ya maji katika vijiji hivyo yenye thamani ya sh. milioni 18 ambazo zimetolewa na Mfuko wa Jimbo ambao mbunge huyo ndiye Mwenyekiti wake.

''Pamoja na kwamba bado hujatangaza rasmi nia ya kugombea nafasi nyeti ya urais ili kurithi mikoba ya Rais Jakaya Kikwete, sisi tuna imani kubwa na utendaji wako na kuona unafaa kuwa Rais wa Awamu ya Tano," alisema mkazi mmoja wa Kijiji cha Nyabila ambaye aliungwa mkono na umati mkubwa wa watu waliokuwepo katika mkutano huo.

Baada ya mkutano huo, Bw. Ngeleja na msafara wake walikwenda Kijiji cha Kagunga kuzindua kisima kilichojengwa katika kitongoji cha Sigu na kupewa baraka kama alizopewa Kijiji cha Nyabila baada ya wananchi kumtaka agombee urais na asipoteuliwa basi agombee ubunge wa jimbo hilo.

"Mheshimiwa Mbunge, wananchi wa Kagunga tunakutaka tena uchukue fomu ili nasi tuonyeshe shukurani zetu kwako, kwa kauli moja tuko tayari kulipa gharama za fomu ya kugombea tena ubunge katika jimbo la Sengerema," walisema wakazi hao katika risala yao kwa mbunge huyo.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...