Skip to main content

Yanga yachoshwa na hujuma Afrika

YANGA imerejea jana kutoka Tunisia ilikotolewa katika Kombe la Shirikisho Afrika, huku ikisema ipo haja kwa Watanzania kuachana na uungwana na ukarimu kwa timu za kigeni zinazokuja kucheza nchinikutokana na mambo wanayofanyiwa timu za Tanzania ugenini.

Aidha, makocha wake wanajivunia timu yao kuonesha umahiri licha ya kucheza na timu ngumu, Etoile Sportive du Sahel.

Kocha Msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa akizungumza na gazeti hili baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jana alasiri, alisema timu yao ilicheza vizuri, lakini hali ilikuwa ngumu kipindi cha pili cha mchezo huo waliofungwa bao 1-0 kwani wenyeji, waliamua ‘kupaki’ basi.

Yanga ilifungwa bao 1-0 na kutolewa katika raundi ya pili baada ya matokeo ya kwanza kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Aprili 18, mwaka huu, kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

“Kama tulivyoeleza kabla ya kuondoka nchini kwamba tumejipanga kwenda kushindana. Vijana walipambana na Watanzania wamejionea wenyewe. Walicheza vizuri na kuonesha uwezo mkubwa,” alisema Mkwasa na kuongeza: “Hali ilikuwa ngumu kipindi cha pili kwa sababu licha ya vijana kuzidi kupambana kwa ku-press zaidi, wenzetu waliamua kurudi nyuma na kuwa wengi zaidi wakilinda lango lao. Hii ilitupa wakati mgumu katika kupenya na kupata bao la kusawazisha.”

Mkwasa anayemsaidia Mholanzi Hans van der Pluijm aliwapongeza wachezaji wa timu hiyo kwa uwezo mkubwa waliouonesha katika mashindano hayo mwaka huu, akisema yalikuwa magumu, lakini wameona mambo ambayo wanatakiwa kuyafanyia kazi ili mwakani wafanye vizuri zaidi.

Kwa kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara, mwakani Yanga itashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika, na Mkwasa anasema: “Tumeona mashindano ya mwaka huu, yapo marekebisho madogo ambayo tutayafanya, lakini tunajivunia kikosi chetu, kina vijana wadogo, lakini wameonesha uwezo mkubwa katika ligi na michuano ya kimataifa.”

Kuhusu mambo wanayokutana nayo katika mechi za ugenini, Mkwasa alisema: “Naamini wakati umefika kwa Watanzania kuacha kuwa waungwana na wakarimu kwa timu zinazokuja hapa. Wenzetu wanatumia mbinu nyingi kutuvuruga kabla ya mechi. “Kwa mfano, mnawekwa uwanja wa ndege masaa matatu, wanawaletea magari mabovu, mnapewa uwanja wa mazoezi kwa muda mfupi. Yaani yote ni kuhakikisha wanawavuruga na kushinda kirahisi. Ni lazima na sisi sasa tuwe na roho ya kikatili.”

Akizungumzia maandalizi ya mechi yao ya kesho ya Ligi Kuu dhidi ya Azam FC, Mkwasa alisema licha ya kutwaa ubingwa, wataingia uwanjani kesho wakiichukulia mechi hiyo kwa uzito mkubwa.

“Hii ni mechi ngumu, Azam FC ni timu nzuri, na juzi wameshindwa, hivyo wataongeza nguvu zaidi katika mechi yetu. Nasi tunajiandaa kwa nguvu zote, tunaichukulia mechi hii kwa umuhimu mkubwa,” alisema Mkwasa.

Yanga ilitwaa ubingwa wa Bara msimu wa 2014/2015 kabla ya kwenda Tunisia kwa kufikisha pointi 55 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine 13 zinazoshiriki ligi hiyo, na imebakiza mechi mbili dhidi ya Azam FC na Ndanda FC.

Kesho itakabidhiwa kombe lake hilo la 25 la ubingwa wa Bara na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara, baada ya mechi hiyo na mabingwa hao wa Bara msimu wa 2013/2014

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...